Tuesday, July 28, 2020
KIFO CHA MKAPA KIMENIUMIZA SANA –MWANA FA
MSANII wa muziki wa Bongo Fleva nchini Hamisi Mwinjuma alimaarufu Mwana FA amesema kifo cha aliyekuwa Rais wa awamu ya tatu Benjamini Mkapa kimemuumiza na ni pigo kubwa kwa wasanii kutokana na mchango wake wa kuanzisha Cosota.
Mwana FA aliyasema hayo leo wakati akizungumza katika wa ibada maalumu ya maombolezo iliyofanyika wilayani Muheza kwenye viwanja wa Jitegemee na kuongozwa na Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo na wananchi wakiwemo viongozi wa dini.
Alisema kutokana na msiba huo mzito ndio maana akaamua kuungana na wananchi wa wilaya ya Muheza katika halfa hiyo kwa sababu katika kipindi chake ndio miongoni mwa taasisi aliyonzisha katika kusimamia haki za wasanii.
Msanii huyo alisema Cosota ni taasisi inayoshughuli na haki miliki za wasanii tokea ilipoanzishwa 1996 na imekuwa na mchango mkubwa kwani kabla ya hapo kazi za wasanii zilikuwa huwezi kumpeleeka mtu mahakamani.
Hata hivyo alisema kutokana na hilo wana mshukuru Hayati Mkapa kutokana na mambo makubwa aliyowafanyia wasanii hapa nchini ambayo yamekuwa na tija kubwa kwao .
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...