WAKULIMA kisiwani Pemba wametakiwa kuchangamkia fursa ya uwepo na kiwanda cha kutengeneza unga wa sembe kisiwani humo cha KANGAROO SUPER SEMBE kwa kuwekeza katika kilimo cha mahindi ili kukidhi mahitaji ya kiwanda hicho, ambacho kinahitaji zaidi ya tani 50 kwa mwezi.
Ushauri huo kwa wakulima umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Wete Kepteni Khatib Khamis Mwadini wakati wa ziara yake kwenye kiwanda hicho ambapo amewataka wakulima kuwekeza zaidi kwenye kilimo cha Mahindi kwani mbali na kuzalisha ajira pia soko lake ni la uhakika.
Amesema kuwa ujenzi wa kiwanda hichi ni kuunga mkono juhudi za serikali katika kuelekea kwenye uchumi wa viwanda
Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho Ali abdalla sharif amesema wanalazimika kufuata malighafi nje ya Kisiwa cha Zanzibar kutokana na kutokuwepo wa malighafi hiyo visiwani humo.
Baadhi ya wananchi wamekizungumzia uwepo wa kiwanda hicho wamesema utawapunguzia gharama wafanyabiashara ya kufuata unga wa sembe nje ya Kisiwa hicho na kuwataka wananchi kuhamasika kulima kilimo cha mahindi.
Kiwanda hicho kwa siku kinazalisha tani themanini(80) ambazo hata hivyo hazikidhi mahitaji ya soko la ndani.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
