WAKULIMA kisiwani Pemba wametakiwa kuchangamkia fursa ya uwepo na kiwanda cha kutengeneza unga wa sembe kisiwani humo cha KANGAROO SUPER SEMBE kwa kuwekeza katika kilimo cha mahindi ili kukidhi mahitaji ya kiwanda hicho, ambacho kinahitaji zaidi ya tani 50 kwa mwezi.
Ushauri huo kwa wakulima umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Wete Kepteni Khatib Khamis Mwadini wakati wa ziara yake kwenye kiwanda hicho ambapo amewataka wakulima kuwekeza zaidi kwenye kilimo cha Mahindi kwani mbali na kuzalisha ajira pia soko lake ni la uhakika.
Amesema kuwa ujenzi wa kiwanda hichi ni kuunga mkono juhudi za serikali katika kuelekea kwenye uchumi wa viwanda
Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho Ali abdalla sharif amesema wanalazimika kufuata malighafi nje ya Kisiwa cha Zanzibar kutokana na kutokuwepo wa malighafi hiyo visiwani humo.
Baadhi ya wananchi wamekizungumzia uwepo wa kiwanda hicho wamesema utawapunguzia gharama wafanyabiashara ya kufuata unga wa sembe nje ya Kisiwa hicho na kuwataka wananchi kuhamasika kulima kilimo cha mahindi.
Kiwanda hicho kwa siku kinazalisha tani themanini(80) ambazo hata hivyo hazikidhi mahitaji ya soko la ndani.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...