Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameyataka Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini kuzingatia Uwazi katika matumizi ya fedha za wafadhili ili kufanikisha malengo ya fedha hizo ambayo ni kuleta maendeleo kwa Wananchi.
Waziri Ummy ameyasema hayo leo (17/06/2020) jijini Doddoma wakati akizindua Muongozo wa uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Tanzania Bara ambapo amesema fedha nyingi zinaingia nchini kwa ajili ya kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo lakini baadhi ya mashirika hayaweki wazi takwimu za mapato na matumizi fedha hizo.
Hata hivyo, Waziri Ummy amesema lengo la mwongozo sio kuyabana Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini bali ni kuhakikisha Wananchi wananufaika na fedha zilizoombwa na Mashirika hayo kwa ajaili maendeleo ya wananchi husika.
Akitoa Mfano, amesema katika Kipindi cha Mwezi Desemba, 2018 hadi Mei 2020 Jumla shilingi Trillioni 3.9 ziliingia nchini kupitia Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kwa ajili ya kutekeleza miradi ya mbalimbali ya maendeleo katika sekta mbalimbali.
"Lazima tujue Mashirika yanaingiza kiasi gani cha fedha na zinatumikaje katika kuleta maendeleo kama ilivyokusudiwa katika maombi ya fedha hizo" alisisitiza Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy ameyaelekeza Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini kuzingatia maelekezo ya muongozo huo, kwa kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia utaalamu wa Kisekta kwa kila afua itakayokuwa inatekelezwa na mashirika hayo, ikiwa ni pamoja na kuomba vibali kutoka kwenye Sekta husika.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara wa Afya- Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu amesema kuwa Muongozo huo utaimarisha mazingira na jitihada za kuboresha ya ufanyaji kazi wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ili yaweze kutoa machango wake katka maendeleo ya taifa.
"Katika Muongozo huu umeeleza kwa kifupi Sheria, taratibu na kanuni zinazotakiwa kufuatwa na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ili kuhakikisha yanatimiza wajibu wake na kutekeleza miradi mbalimbali ya Maendeleo.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Dkt. Richard Sambaiga amesema kuwa Muongozo huo utasaidia Uratibu mzuri kwa Mashirika hayo kutokana na ongezeko la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ambalo limeongeza changamoto za kiutendaji kwa Mashirika yasiyo ya kiserikali nchini.
Amesema awali kulikuwa na changamoto ya usajili na uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kutokana na kuwajibika kwa Mamlaka zaidi ya moja na hivyo kusababisha usumbufu kwa wadau.
Source
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Siku moja baada ya Israel kusema kuwa inazidisha uvamizi wake wa ardhini nchini Lebanon, Hezbollah inadai iliwafukuza wanajeshi wa Israel ...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...