Monday, June 1, 2020

Boti lazama nchini Ghana, watu 24 hawajulikani walipo

Watu  24 hawajulikani walipo baada ya boti  kuzama  katika Ziwa Volta nchini Ghana.

Mtu mmoja amefariki baada ya mashua yao kuzama na wengine 24 hawajulikani walipo baada ya ajali hiyo kutokea katika ziwa Volta nchini Ghana.

Kulinagana na taarifa zilizotolewa na  shirika linalohusika na   msaada katika matukio ya dharura na uokozi NADMA , mashua hiyo iliozama ilikuwa safarini kutokea katika   mji wa Agalakope ikielekea  katika kijiji cha Dzemeni nchini Ghana.

Kwa mujibu wa ripoti iliotolewa kuhusu ajali hiyo, mashau hiyo imezama kutokana na kubeba abiria wengi kuliko uwezo wake.

SHuhuli za kuwatafuta watu waliozama katika ajli hiyo zinaendelea.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...