Monday, April 27, 2020
New Zealand yatangaza kuangamiza virusi vya corona
New Zealand inasema kwamba imezuia maambukizi ya Covid 19 katika jamii hatua ambayo inamaanisha kwamba wameangamiza virusi hivyo.
Huku wagonjwa wapya wachache wakiripotiwa katika siku kadhaa - mmoja siku ya Jumapili - Waziri mkuu Jacinda Ardem amesema kwamba virusi hivyo vimeangamizwa kabisa.
Lakini maafisa wameonya dhidi ya kupunguza kasi dhidi ya virusi hivyo, wakisema kwamba haimaanishi kwamba visa vya ugonjwa huo vimeisha kabisa.
Habari hiyo inajiri saa chache kabla ya New Zealand kuondoa masharti yake makali ya kukaribiana miongoni mwa raia wake.
Kuanzia Jumanne , biashara zisizo na muhimu mkubwa , huduma za Afya na elimu zinatarajiwa kufungua milango yake tena.
Watu wengi hatahivyo watatakiwa kusalia majumbani kila wakati na kuzuia kukaribiana.
"Tunaufungua uchumi , lakini haturuhusu mikusanyiko ya watu'' , bi Arden alisema katika hotuba hiyo ya serikali ya kila siku kwa umma. News Zealand imeripoti chini ya wagonjwa 1,500 na vifo 19 .
Mkurugenzi mkuu wa Afya nchini New Zealand Ashley Bloomfield alisema kwamba wagonjwa wachache wanaoripotiwa katika siku za hivi karibuni wanatupatia motisha kwamba tunaafikia lengo letu la kuangamiza ugonjwa huu.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
