Thursday, April 30, 2020
Jumuiya ya Mawakili Zanzibar yatuma rambirambi kufuatia kifo cha Jaji Mstaafu Augustine Ramadhani
Jumuiya ya Mawakili Zanzibar (ZLS) imepokea kwa masikitiko na huzuni kubwa taarifa za vifo vya Majaji Wakuu Wastaafu wawili wa Zanzibar ambao ni Mh.Augustine Lawrence Ramadhan na Mh.Ali Haji Pandu pamoja na kadhi Mkuu Mstaafu wa Zanzibar Shk.Habib Ali Kombo amabao wote kwa pamoja wamefariki ndani ya wiki moja katika mwezi wa April,2020.
Marehemu wote watatu walitoa mchango mkubwa katika kuujenga na kuuimarisha Mhimili wa Mahkama ambao ndio wenye dhamana ya utoaji haki katika nchi yetu.
Aidha waliitumikia Zanzibar kwa bidii na uadilifu mkubwa ambao unaonekana kwenye hukumu zao mbalimbali na jitihada zao za kusomesha vijana elimu ya sharia na sheria.
Marehemu watakumbukwa kwa kujituma kwao na kusimamia sheria katika utekelezaji wa utoaji haki katika nyakati na mazingira tofauti.
Kufuatia msiba huu Jumuiya ya Mawakili Zanzibar(ZLS) inaomba ikupendeze kupokea rambirambi zake kwako ukiwa Mkuu wa Mhimili wa Mahkama ambao marehemu wote waliufanyia kazi kwa juhudi, busara na maarifa makubwa.
Aidha, Jumuiya inaungana na wanafamilia na Taifa kwa ujumla katika kuomboleza misiba hii pamoja na kuwaombea wanafamilia kuwa na busra katika kipindi hiki kigumu.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
