Friday, March 27, 2020
Wizara ya Elimu imetoa elimu kwa wafanya kazi wake
Na Thabit Madai
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said amesema Wizara yake imeamua kuwapatia Elimu wafanyakazi wake juu ya kujikinga na virusi vya korona.
Amesema kutokana na kuenea kwa kasi kwa virusi hivyo duniani ipo haja ya kuwaelimisha watendaji wa Wizara hiyo ili waweze kufanyakazi kwa umakini.
Akizungumza wakati wa utoaji wa elimu ya Afya katika viwanja vya Wizara hiyo Mazizini Mjini Unguja Mhe Simai amewataka wafanyakazi hao kuwa makini pamoja na kuifanyia kazi elimu waliyoipata na kuwa mabalozi wazuri wa kuwaelimisha wengine ili kuweza kujikinga na maradhi hayo.
Nae Afisa mahusiano kutoka kitengo Cha Elimu ya Afya Bwana Ahmed Mohamed amesema virusi vya ugonjwa wa Korona husambaa haraka, hivyo ni vizuri kwa kila mmoja kuchukua tahadhari ya hali ya juu ili kuepuka maambukizo ya virusi vya korona.
Amesema virusi husambaa kwa kushikana au kugusa sehemu za vitasa, funguo, ambavyo alieathirika aliaacha virusi huku maambukizi,na dalili zake ni kupata homa Kali na kifua kikavu, kuumwa na kichwa Sana na machofu mwilini.
Aidha amesema Serikali ya Tanzania imetangaza rasmi kwa kila raia atakaeingia nchini kutoka nchi iliopata maambukizi, lazima awekwe kwenye Maandalizi Maalum kwa muda wa siku kumi na nne.
Nao Wafanyakazi wa Wizara ya Elimu Zanzibar wameishukuru Wizara yao kwa hatua waliochukua viongozi wao kwa kuwapa Elimu watendaji wake, ambayo imewasaidia kujua Kinga na athari za virusi vya korona.
Aidha wametoa wito kwa wazazi kuwasimamia watoto wao juu ya kutozurura ovyo na badala yake kujisomea majumbani mwao ili kuwaepusha na maambukizi hayo.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
