Zoezi la kujifungua linafariji na kuchosha pia, ni la faraja sana kwa kuwa linakufanya uwe mama? Wiki 4 za mwanzo kwa mzazi zinaweza kuwa katika kumbukumbu zako kwa muda mrefu kwakuwa ni wiki za 'majimaji' tu – jasho, kunyonyesha na haja ndogo kutoa majimaji yote ya ziada mwilini mwako. Inashangaza hata kama mtu utakuwa na hamu ya kufanya mapenzi katika kipindi hicho.
Madaktari wanasema kuwa mwili wa mwanamke unahitaji wiki 6 kurudi kwenye hali yake ya kawaida. Katika kipindi hiki cha wiki 6, mfupa wa nyonga na uti wa mgongo hurudi kwenye hali yake ya awali. Homoni zako pia zinajirekebisha sambamba na misuli iliyopo kwenye sakafu ya nyonga kupumzika wakati ikirudi kwenye hali yake iliyokuwa nayo mwanzo kabla ya kazi kubwa iliyotoka kuifanya ya kumbeba mtoto na kusaidia kwenye kumtoa wakati wa kujifungua.
Kwahiyo, mpaka kitakapofika kipindi hiki cha wiki 6, unashauriwa kutofanya mapenzi, lakini haimaanishi kwamba huwezi kufanya mambo mengine kama kumbusu, kumshikashika, au kumnyonya mwanaume wako, na yeye kukufanyia hivyo hivyo. Wanawake wengine wanasema kuwa chuchu zao huwa na hisia sana kutokana na kunyonyesha kiasi kwamba wanaweza kufika kileleni kwa kushikwa chuchu tu.
Lakini kuhusu dawa za kuzuia kubeba mimba katika kipindi hiki, mnashauriwa muwe na tahadhari kuhusu kutumia njia yoyote itayoathiri mfumo wa homoni. Hii ni kwa sababu itaathiri sana kiwango na ubora wa maziwa na itamsababishia mtoto kutopata lishe inayotakiwa. Pia, vidonge vyenye oestrogen vimethibitishwa kusababisha kupungua kwa kiwango cha maziwa kwa mama anayenyonyesha, na mara nyingine hupunguza ghafla sana.
Shirika la Afya Duniani linasisitiza mtoto anywe maziwa tu kwa muda usiopungua miezi 6 kisha uendelee kumnyonyesha mpaka atakapofikisha miaka miwili. Wazazi wengi wanaona hii inawatesa na wengi wao wanasema kwamba miezi 6 ya mwanzo ni muhimu sana.
Unashauriwa uzungumze na daktari wako kuhusu muda gani unaweza kurudia kufanya mapenzi na njia za kutumia kujikinga na mimba ya haraka na pia umuulize hasa kuhusu kutumia dawa zenye progesterone na madhara yake kwako. Vidonge hivi vinaathiri maziwa (kwa wingi na ubora) kwa kiwango kidogo zaidi ukilinganisha na vidonge vyenye oestrogen.
Mwili wako umefanya kazi kubwa sana ya kuleta kiumbe duniani. Sio tu kwa sababu ni utambulisho wako na kukufanya uitwe 'mama' na chochote utachofanya kitakachokufurahisha, utashangaa jinsi ulivyo na sehemu nyingi zinazoweza kukufanya upate raha.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...