Zoezi la kujifungua linafariji na kuchosha pia, ni la faraja sana kwa kuwa linakufanya uwe mama? Wiki 4 za mwanzo kwa mzazi zinaweza kuwa katika kumbukumbu zako kwa muda mrefu kwakuwa ni wiki za 'majimaji' tu – jasho, kunyonyesha na haja ndogo kutoa majimaji yote ya ziada mwilini mwako. Inashangaza hata kama mtu utakuwa na hamu ya kufanya mapenzi katika kipindi hicho.
Madaktari wanasema kuwa mwili wa mwanamke unahitaji wiki 6 kurudi kwenye hali yake ya kawaida. Katika kipindi hiki cha wiki 6, mfupa wa nyonga na uti wa mgongo hurudi kwenye hali yake ya awali. Homoni zako pia zinajirekebisha sambamba na misuli iliyopo kwenye sakafu ya nyonga kupumzika wakati ikirudi kwenye hali yake iliyokuwa nayo mwanzo kabla ya kazi kubwa iliyotoka kuifanya ya kumbeba mtoto na kusaidia kwenye kumtoa wakati wa kujifungua.
Kwahiyo, mpaka kitakapofika kipindi hiki cha wiki 6, unashauriwa kutofanya mapenzi, lakini haimaanishi kwamba huwezi kufanya mambo mengine kama kumbusu, kumshikashika, au kumnyonya mwanaume wako, na yeye kukufanyia hivyo hivyo. Wanawake wengine wanasema kuwa chuchu zao huwa na hisia sana kutokana na kunyonyesha kiasi kwamba wanaweza kufika kileleni kwa kushikwa chuchu tu.
Lakini kuhusu dawa za kuzuia kubeba mimba katika kipindi hiki, mnashauriwa muwe na tahadhari kuhusu kutumia njia yoyote itayoathiri mfumo wa homoni. Hii ni kwa sababu itaathiri sana kiwango na ubora wa maziwa na itamsababishia mtoto kutopata lishe inayotakiwa. Pia, vidonge vyenye oestrogen vimethibitishwa kusababisha kupungua kwa kiwango cha maziwa kwa mama anayenyonyesha, na mara nyingine hupunguza ghafla sana.
Shirika la Afya Duniani linasisitiza mtoto anywe maziwa tu kwa muda usiopungua miezi 6 kisha uendelee kumnyonyesha mpaka atakapofikisha miaka miwili. Wazazi wengi wanaona hii inawatesa na wengi wao wanasema kwamba miezi 6 ya mwanzo ni muhimu sana.
Unashauriwa uzungumze na daktari wako kuhusu muda gani unaweza kurudia kufanya mapenzi na njia za kutumia kujikinga na mimba ya haraka na pia umuulize hasa kuhusu kutumia dawa zenye progesterone na madhara yake kwako. Vidonge hivi vinaathiri maziwa (kwa wingi na ubora) kwa kiwango kidogo zaidi ukilinganisha na vidonge vyenye oestrogen.
Mwili wako umefanya kazi kubwa sana ya kuleta kiumbe duniani. Sio tu kwa sababu ni utambulisho wako na kukufanya uitwe 'mama' na chochote utachofanya kitakachokufurahisha, utashangaa jinsi ulivyo na sehemu nyingi zinazoweza kukufanya upate raha.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
