Friday, February 7, 2020
Mwamuzi Aliyeruhusu Goli la Kagera Afungiwa Miaka Mitatu
KAMATI ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imepitia mwenendo wa matukio ya ligi na kufanya maamuzi mbalimbali ikiwemo utoaji adhabu kwa wahusika.
Katika kikao hicho cha Februari 03, 2020, kamati imeridhia kumfungia miaka mitatu mwamuzi msadizi namba mbili wa mchezo namba 150: kati ya Simba SC (3-2) Namungo FC Kassim Safisha kwa kushindwa kutafsiri sheria ya kuotea (offside) katika mechi hiyo.
Wakati huo huo Mwamuzi Meshack Suda ameandikiwa barua ya kukumbushwa kufanya majukumu yake kwa umakini zaidi katika mechi namba 157 iliyochezwa Januari 30, 2020 kati ya Azam FC (1-1) Mtibwa FC kwenye Uwanja wa Taifa.
Vile vile katika mchezo huo Kamishina Abdallah Zongo ameondolewa kwenye orodha ya makamishina kutokana na kutoa taarifa yenye mapungufu huku adhabu hiyo ikitafsiriwa kulingana na kanuni namba 40(1) kuhusu Udhibiti kamishina wa mchezo.
Katika mechi namba 75A kati ya Friends Rangers (0-1) Dodoma FC, Kiongozi wa Klabu ya Friends Rangers Heri Chibakasa amepelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) kwa kosa la kupigana na mashabiki wa timu pinzani.
Aidha TPLB imetoa adhabu kwa Mwamuzi Salum Mkole ambaye amefungiwa miezi mitatu kwa kosa la kuonesha udhaifu katika usahihi wa kutoa kadi katika mechi namba 29A iliyochezwa Januari 31, 2020 kati ya Dar City Fc (1-0) African Sports, katika dimba la Uhuru.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
