Monday, January 13, 2020
Chama Cha Wamiliki wa Mabasi (TABOA) mbioni kuanza kukatisha tiketi Kielectroniki
Na Ezekiel Mtonyole, Dodoma
Chama cha wamiliki wa mabasi nchini (TABOA)kimesema kipo katika hatua nzuri kukamilisha zoezi la kuanza kukatisha tiketi kwa njia ya kielektroniki ili kupunguza msongamano na usumbufu kwa abiria hasa wakati wa msimu wa sikukuu.
Akizungumza na Muungwana blog Katibu wa TABOA Enea Mruto amesema baada ya kikao chao na mamlaka ya mapato nchini TRA kufikia makubaliano taratibu za ukatishaji tiketi kwa njia ya elektroniki unaarajia kuanza mwezi ujao kwa mabasi yote.
"Kama TRA hawatatuangusha kile tulichokubaliana nao basi mpango huo utaanza rasmi mwezi ujao tunahitaji kufanya kazi kwa kwenda na teknolojia mpya kuondoa usumbufu kwa wateja wetu "amesema Mruto.
Amesema wakakamilisha baadhi ya taratibu mpango huo utazinduliwa rasmi na kuwekwa agizo kwa mabasi kuanza kutumia njia hiyo ambayo inawarahisishia wateja kupata tiketi rahisi au kuweka booking kwa njia ya mtandao.
Amesema licha ya kuwa baadhi ya kampuni zimejaribu kuanza mpango huo ila rasmi itakuwa mwezi ujao kwa mabasi yote kuanza kutumia mfumo huo utakao warahisishia wateja wao kupata tiketi kwa njia salama.
Akizungumzia agizo la Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Mhandisi Atashasta Nditiye, kuhakikisha mabasi yote yasiyokuwa na vibali kusafirisha vifurushi.
Amesema hata katika mkutano wao wamiliki walisisitiza agizo hilo ili kuendana na Sheria zinavyohitaji na kwenda sambamba na Serikali inavyoagiza.
"TABOA tunatekeleza agizo hilo atakayekiuka atakupambana na mkono wa sheria hivyo kila mmoja anapaswa kutekeleza sheria, "amesema.
Katika hatua nyingine Mrutu amesema moja ya mikakati waliojiwekea ni kuhakikisha wanapunguza ajali za barabarani kwa kuhimiza umakini katika kampuni za mabasi hususa ni kwa madereva kutii Sheria na taratibu zilizowekwa.
Amesema wao kama TABOA watakuwa wakisisitiza wamiliki wa mabasi kufanya ukaguzi katika vyombo vyao vya moto ili kunusuru ajali zinazotokea mara kwa mara.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...