Monday, January 13, 2020
Chama Cha Wamiliki wa Mabasi (TABOA) mbioni kuanza kukatisha tiketi Kielectroniki
Na Ezekiel Mtonyole, Dodoma
Chama cha wamiliki wa mabasi nchini (TABOA)kimesema kipo katika hatua nzuri kukamilisha zoezi la kuanza kukatisha tiketi kwa njia ya kielektroniki ili kupunguza msongamano na usumbufu kwa abiria hasa wakati wa msimu wa sikukuu.
Akizungumza na Muungwana blog Katibu wa TABOA Enea Mruto amesema baada ya kikao chao na mamlaka ya mapato nchini TRA kufikia makubaliano taratibu za ukatishaji tiketi kwa njia ya elektroniki unaarajia kuanza mwezi ujao kwa mabasi yote.
"Kama TRA hawatatuangusha kile tulichokubaliana nao basi mpango huo utaanza rasmi mwezi ujao tunahitaji kufanya kazi kwa kwenda na teknolojia mpya kuondoa usumbufu kwa wateja wetu "amesema Mruto.
Amesema wakakamilisha baadhi ya taratibu mpango huo utazinduliwa rasmi na kuwekwa agizo kwa mabasi kuanza kutumia njia hiyo ambayo inawarahisishia wateja kupata tiketi rahisi au kuweka booking kwa njia ya mtandao.
Amesema licha ya kuwa baadhi ya kampuni zimejaribu kuanza mpango huo ila rasmi itakuwa mwezi ujao kwa mabasi yote kuanza kutumia mfumo huo utakao warahisishia wateja wao kupata tiketi kwa njia salama.
Akizungumzia agizo la Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Mhandisi Atashasta Nditiye, kuhakikisha mabasi yote yasiyokuwa na vibali kusafirisha vifurushi.
Amesema hata katika mkutano wao wamiliki walisisitiza agizo hilo ili kuendana na Sheria zinavyohitaji na kwenda sambamba na Serikali inavyoagiza.
"TABOA tunatekeleza agizo hilo atakayekiuka atakupambana na mkono wa sheria hivyo kila mmoja anapaswa kutekeleza sheria, "amesema.
Katika hatua nyingine Mrutu amesema moja ya mikakati waliojiwekea ni kuhakikisha wanapunguza ajali za barabarani kwa kuhimiza umakini katika kampuni za mabasi hususa ni kwa madereva kutii Sheria na taratibu zilizowekwa.
Amesema wao kama TABOA watakuwa wakisisitiza wamiliki wa mabasi kufanya ukaguzi katika vyombo vyao vya moto ili kunusuru ajali zinazotokea mara kwa mara.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
