Saturday, December 14, 2019
Aliyeachiwa kwa msamaha wa Rais azua taharuki stand ya Bukoba auwa mmoja ajeruhi watano
Na Clavery Christian Bukoba Kagera.
Jeshi la polisi mkoani Kagera linaendelea na uchunguzi wa tukio la mauaji ya watu wawili na majeruhi watano baada ya mtu mmoja anayesadikika kuwa ni mmoja kati ya wafungwa waliotoka jera kwa msamaha wa Rais kuwavamia na kuwashambulia kwa kuwachoma visu katika maeneo mbalimbali ya mwili katika eneo la stand kuu ya mabasi bukoba na kusababisha taharuki kubwa kwa raia.
Majeruhi watano ambao ni wananchi wa kawaida waliojeruhiwa na mtu huyo katika tukio hilo watatu wamelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa - Bukoba na hali zao zinaendelea vizuri japo kuwa mmoja kati yao alipata majeraha makubwa.
Kwa mujibu wa mashuhuda wanaeleza kwamba jana tarehe 13/12/2019 majira ya saa 03:00 usiku maeneo ya stand kuu ya mabasi Bukoba ghafla mtu mmoja asiyefahamika majina yake majina yake mwenye kati ya umri wa miaka 30-35 jinsia mwanaume alivamia watu waliokuwa hapo stand na kuanza kuwachoma watu visu na mtu wa kwanza kuanza kumchoma alikuwa Godfrey Gobadi miaka 30-35 ni mhaya dereva wa bajaji ambaye alimchoma kisu tumboni na kumsababishia kifo papo hapo.
Aidha mtu huyo alizidi kusababisha hofu na taharuki kubwa kwa watu wa eneo hilo alipoendelea kuwavamia na kuwachoma visu watu wengine na kujeruhi watu watano.
Baada ya mtuhumiwa kufanya vitendo hivyo wananchi wenye hasira kali walimvamia na kuanza kumshambulia na kumuumiza vibaya na baadae askari polisi waliokuwa doria waliweza kufika katika eneo hilo na kufanikiwa kumuokoa mtuhumiwa asiendelee kushambuliwa lakini alifariki wakati akipelekwa hospitalini.
Kamanda wa polisi mkoani Kagera Revocatus Malimi amesema kuwa chanzo cha tukio hilo hakijafahamika na uchunguzi bado unaendelea.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
