Saturday, December 14, 2019
Aliyeachiwa kwa msamaha wa Rais azua taharuki stand ya Bukoba auwa mmoja ajeruhi watano
Na Clavery Christian Bukoba Kagera.
Jeshi la polisi mkoani Kagera linaendelea na uchunguzi wa tukio la mauaji ya watu wawili na majeruhi watano baada ya mtu mmoja anayesadikika kuwa ni mmoja kati ya wafungwa waliotoka jera kwa msamaha wa Rais kuwavamia na kuwashambulia kwa kuwachoma visu katika maeneo mbalimbali ya mwili katika eneo la stand kuu ya mabasi bukoba na kusababisha taharuki kubwa kwa raia.
Majeruhi watano ambao ni wananchi wa kawaida waliojeruhiwa na mtu huyo katika tukio hilo watatu wamelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa - Bukoba na hali zao zinaendelea vizuri japo kuwa mmoja kati yao alipata majeraha makubwa.
Kwa mujibu wa mashuhuda wanaeleza kwamba jana tarehe 13/12/2019 majira ya saa 03:00 usiku maeneo ya stand kuu ya mabasi Bukoba ghafla mtu mmoja asiyefahamika majina yake majina yake mwenye kati ya umri wa miaka 30-35 jinsia mwanaume alivamia watu waliokuwa hapo stand na kuanza kuwachoma watu visu na mtu wa kwanza kuanza kumchoma alikuwa Godfrey Gobadi miaka 30-35 ni mhaya dereva wa bajaji ambaye alimchoma kisu tumboni na kumsababishia kifo papo hapo.
Aidha mtu huyo alizidi kusababisha hofu na taharuki kubwa kwa watu wa eneo hilo alipoendelea kuwavamia na kuwachoma visu watu wengine na kujeruhi watu watano.
Baada ya mtuhumiwa kufanya vitendo hivyo wananchi wenye hasira kali walimvamia na kuanza kumshambulia na kumuumiza vibaya na baadae askari polisi waliokuwa doria waliweza kufika katika eneo hilo na kufanikiwa kumuokoa mtuhumiwa asiendelee kushambuliwa lakini alifariki wakati akipelekwa hospitalini.
Kamanda wa polisi mkoani Kagera Revocatus Malimi amesema kuwa chanzo cha tukio hilo hakijafahamika na uchunguzi bado unaendelea.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...