Waziri wa Maji Prof, Makame Mbarawa amewaagiza wakandarasi wanaojenga mradi wa maji ya Ziwa victoria kutoka kahama hadi Isaka kwenda wa mkuu wa wilaya ya kahama kuandika makubaliano maalumu ambayo yataonesha ni lini watakamilisha miradi hiyo baada ya kushindwa kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.
Uamuzi huo umetolewa jana na Prof.Mbarawa baada ya kupokea taarifa za kutokamilika kwa mradi huo kutokamilika kwa wakati huku wakiendelea kutoa ahadi za uongo.
Mbarawa amefafanua kuwa Wakandarasi hao wameshindwa kutimiza mashariti ya mkataba walioingia na serikali hivyo hawatakuwa na nafasi tena ya kuendendelea kutokamilisha mradi huo licha ya kuwa fedha wameshalipwa na serikali.
Amesema serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais, Dk John Magufuli haitakubali kuendelea kuwakumbatia wakandarasi wazembe ambao wanakwamisha shughuli za maendeleo ya wananchi katika maeneo wanayoishi.
Kwa upande wake Ezekiel Maige ni mbunge wa jimbo la Msalala amemuomba Waziri Mbarawa kuwabana wakandarasi hao ili mradi huo ukamilike kwa wakati ili kuwawezesha wananchi kupata maji safi na salama.
Nao baadhi ya wananchi Kurwa Kitunga na Kashindye Singu wa Kata za Mwakata na Mwendakulima waliojitokeza katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Waziri huyo wameomba kujengewa magati ya maji katika vijiji ambavyo kunashida ya maji ili kuwawezesha kuacha kutumia maji ambayo sio safi yanayotumika pamoja na wanyama.
Kampuni zilipewa dhabuni ya kujenga mradi huo ni pamoja na Oriental conslin limited na Changs ambazo zimepewa kandarasi hiyo yenye thamani ya zaidi ya bilioni 22 ambapo walitakiwa kukamilisha mradi huo mwezi june mwaka huu.
Bado Waziri Mbarawa anaendelea na ziara yake ya kikazi ya siku 4 mkoani shinyanga kukagua miradi mbalimbali ya maji.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...