Wednesday, July 10, 2019
Hospital mpya ya rufaa Njombe yaanza kutoa huduma
Na Amiri kilagalila-Njombe
Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu amefungua zoezi la utoaji wa huduma ya afya katika hospital mpya ya rufaa ya mkoa wa Njombe iliyofunguliwa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania alipokuwa na ziara ya siku tatu kuanzia april 9 mwaka huu mkoani humo.
Akizungumza na wananchi kabla ya kukabidhi hospital hiyo kwa mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher olesendeka amesema kuwa awali mkoa wa Njombe ulikuwa ukitumia hospital ya kibena iliyochini ya halmashauri ya mji wa Njombe kuwa hospital teule ya mkoa.
Ili kuendelea kuboresha na kusogeza karibu huduma za afya mkoani humo waziri Ummy amesema kuwa hospital ya kibena haitoweza kuondolewa kifaa chochote huku akitoa wito kwa halmashauri ya mji wa Njombe kuendelea kuboresha huduma zinazotolewa katika hospital hiyo.
"Hamkufanya makosa halmashauri kutukabidhi hospital ile ya kibena ninyi wenyewe ni mashahidi baada ya kuwa imeteuliwa hospital teule ya mkoa,hali ya utoaji huduma ilibadirika,sasa niseme pale katika hospital hatutaondoa.
chochote,na mimi ni matumaini yangu kwamba halmashauri mtaendelea kuboresha ili ipatikane huduma bora".
Katika hatua nyingine waziri Ummy amemkabidhi site mkandarasi ili kuanza ujenzi wa majengo 7 ya kisasa katika ujenzi wa hatua ya pili na kumpa mkandarasi miezi 8 mpaka 10 na kumpongeza Rais kwa kutoa bilioni 7.65 kwa ajili ya ujenzi huo.
Awali mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka mara baada ya kuishukuru serikali kwa kuzindua huduma katika hospital hiyo,ameagiza halmashauri kuweka utaratibu mzuri wa usafiri ili wananchi waweze kupata huduma kufika katika hospital hiyo.
Mganga mfawidhi wa iliyokuwa hospital ya rufaa ya mkoa wa Njombe kibena Dkt.Winferd Kiambile,amesema miongoni mwa huduma zitakazotolewa katika hospital mpya ni pamoja na kliniki za kibingwa.
"Mh waziri nikuhakikishie kwamba watoa huduma tupo tayari kutoa huduma katika hospital hii,huduma zitakazotolewa ni huduma za OP zote vile vile kuna kliniki za kibingwa,na huduma nyingine nyingi"
Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika uzinduzi huo wamesema kuwa kuanza kutumika kwa hospital hiyo kutawapunguzia gharama kwa kuwa awali walikuwa wakifuata huduma kubwa za rufaa katika mikoa jirani ikiwemo Mbeya na Iringa.
Hospital ya rufaa ya mkoa wa Njombe kwa wagonjwa wa nje, awamu ya kwanza ya ujenzi umegharimu bilioni 3.2
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...




