Thursday, July 4, 2019
Bei za bidhaa mbalimbali zimeshuka visiwani Zanzibar
Na Thabit HamidumZanzibar,
MKUU Wa Kitengo cha bei Khamis Abdulrahman Msham amesema hali ya mfumo wa bei za bidhaa umepungua kutoka asilimia 3.1 hadi kufikia 2.7 kwa mwaka uloishia June 2019 kwa bidhaa mbalimbali zinazotumiwa na wananchi tofauti visiwani Zanzibar.
Hayo ameyasema leo huko katika Ukumbi ya Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Mazizini Mkoa wa Mjini Unguja wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu muendelezo wa kuripoti taarifa za bei kuhusu kushuka kwa bidhaa ikiwemo chakula.
Alisema mfumuko wa bei za bidhaa umepungua ikiwemo chakula kama vile mchele wa mapembe, mchele wa basmati, ndizi na samaki na pia mafuta ya taa.
Aliongeza kusema hali ya uchumi inaimarika vizuri ukilinganisha na nchi nyengine za Afrika Mashariki kwa jinsi kasi ya kupanda imepungua kutokana na uzalishaji uliyo mzuri.
Nae Meneja wa Idara ya Uchumi Tanzania Bank of Tanzania BOT Moto Ng'winganele Lugobi alisema hali ya mfumuko wa bei kwa sasa ni mzuri kutokana na uzalishaji wa mavuno uko vizuri na kuwataka wananchi kuzalisha mavuno kwa wingi.
Kwa upande wa Mhadhiri wa Uchumi kutoka chuo kikuu cha Taifa SUZA Suleiman Msaraka Pinja alisema Serikali ikianza bajeti huweka malengo yake hivyo lengo la mfumko wa bei usizidi ili wananchi waweze kumudu bei za bidhaa.
Hivyo lengo limetimia mfumo wa bei umeshuka na kuwataka wananchi waendelee kuzalisha chakula kwa utaalamu zaidi kwani wakifanya hivyo mfumko wa bei hautokuwa mkubwa.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
