Karibu watu 100 wameripotiwa kuuawa katika kijiji cha watu wa jamii ya Dogon nchini Mali.
Shambulio hilo limefanyika katika kijiji cha Sobale Kou, karibu na mji wa Sanga, kwa mujibu wa kituo cha habari cha Ufaransa RFI.
Miili ya waliouawa imeteketezwa moto, anasema afisa katika eno hilo na kuongeza kuwa shughuli ya kutafuta miili zaidi inaendelea.
Kumeshuhudiwa visa kadhaa vya mashambulio nchini Mali katika miezi ya hivi karibuni na baadhi ya mashambulio hayo yanasadikiwa kutekelezwa na makundi ya kijihadi.
Mzozo kati ya wawindaji wa jamii ya Dogon na wafugaji wa jamii ya Fulani umekuwa ukiibuka mara kwa mara.
Meya wa mji wa jiji la Bankass, Moulaye Guindo, ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa watu wa jamii ya Fulani kutoka wilaya hiyo walishammbulia Sobane-Kou after giza likiingia.
Afisa wa eneo la Koundou, ambalo linajumuisha kijiji kilichoshambuliwa, ameliambia shirika la habari la AFP kuwa: " sasa hivi tunathibitisha vifo vya watu 95. Miili imechomwa na bado tunaendelea kutafuta maiti zingine."
Mapigano kati ya jamii hizo mbili imeongezeka tangu wanamgambo wa kiislam walipovamia eneo la kaskazini mwa Mali mwaka 2012.
Mwezi machi mwaka huu zaidi ya wanavijiji 130 wa jamii ya Fulani waliuawa na watu waliyokuwa wamejihami na amabo walidaiwa kuvalia mavazi ya kitamaduni ya wawindaji wa Dogon.
Tofauti kati ya jamii ya Fulani na Dogon ilisuluhishwa kupitia mashauriano ya amani lakini ghasia zilizosambaa maeneo ya kati ya Mali mwaka 2015 -ziliathiri udhibiti wa serikali hali iliyosababisha kuingizwa kwa silaha.
Pande zote mbili zinalaumiana kwa uchokozi na kuanzisha mapigano.
Source
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
