Saturday, June 8, 2019
Tabia za Wanawake Kuchukiana Bila Sababu..Nini Tatizo?
Ni hivi kwenye ofisi ninayofanya kazi tuko watumishi kama 15 hivi,kati ya hao wanawake tuko saa watano pamoja na ps,walobaki ni wanaume.
Basi kuna kipindi tulipewa zawadi ofisini,nami nilikuwepo miongoni mwa waliopata,tukiwa wanawake wawil tu tuliobahatika ,nikajipost kwenye group ya ofisini wanaume almost wote walikuwa happy na kunipongeza,ikaja kwa wanawake Sasa,mtu unakutana naye koridoni anakuuliza nimeona bana umepewa cheti,unamjibu ndio,anakwambia hongera huku ikiambatana na kicheko Cha kebehi na kejeli.
Ukija kwenye groups za wasap, comments wanazotoa wanaume kwetu wanawake si za kubeza,hata kama kukukosoa atakukosoa kistaarabu.Ila wanawake mtu atoa comments kama mna ugomvi,ama aweza comment neno la kukudhalilisha ilmradi usijisikie vizuri.Hadi wajiuliza ,tatizo nini?
Kuna wakati mwenzetu mmoja alikuwa mjamzito, jamaa mmoja wa ofisin akapiga naye picha akaipost kwa group,most of men walikuwa happy na walikuwa wanacomment positively,na matani ya hapa na pale,ila upande wa wanawake sasa wakatoa maneno ya kejeli na kuonyesha kutofurahia hilo jambo,as if wamechangia mume .Mwingine akaandika ,,ahhh mama kijaaa hongera bwana,then hehehehe halooo
,Like what the f@ck?
Hata kwenye ishu za deals ni mara chache,mwanamke akushirikishe hata kama una uwezo wa kulifanikisha,but kwa upande wa wanaume wako so smooth na washirikishaji wazuri.Tena wanawake hao wakigundua kuna kaishu unafatilia yuko radhi hata akuharibie kwa client,ili tu mkose wote.
Ishu ni nyingi,ila wanawake mostly hatupendani maofisini,Hatuko professional mostly,Tunasemana vibaya,tunaoneana wivu wa kijinga (siyo wa kimaendeleo),tunachafuana Wala hatusapotiani kwenye ishu positive.Nashindwa elewa tatizo ni nini.
So swali ni kwanini wanawake hatupendani?ni nature?Ni laana?Na suala la kutaka unnecessary competition na wanawake wengine sababu ni nini?
JF
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
