Friday, June 21, 2019
Serikali yapiga marufuku ufuta kuuzwa kwa walanguzi
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge amepiga marufuku wananchi kuuza ufuta kwa walanguzi badala yake wanatakiwa kuuza kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani.
Dk Mahenge alitoa agizo hilo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Keikei Tangini kata ya Keikei baada ya kusikia malalamiko kwa wananchi kuuza ufuta kwenye maghala kwa mtindo wa skakabadhi ghalani.
Pia alimuagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto kupanga askari na kuhakikisha wanakagua magari yaliyobeba ufuta kabla haujauzwa kwenye minada kupitia kwenye maghala yasipite kwenda kuuzwa Dodoma mjini.
Pamoja na hayo alimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa Vijijini, Yusufu Mgambo kuhakikisha anakusanya ufuta wa wananchi akiwa na uhakika wa kuwalipa ndani ya siku mbili badala ya kukusanya na kukaa nao bila kuwalipa.
Dk Mahenge alisema ufuta unatakiwa kuuzwa kwa mnada baada ya kuhifadhi kwenye maghala na wananchi ambao watakuwa wamelipwa fedha zao badala ya kuuza kwa walanguzi ambao wanaifanya pia halmashauri hiyo kukosa mapato.
Alisema mfumo huo wa stakabadhi ghalani ni agizo la serikali kupitia vyama vya ushirika kwa mikoa yote ambayo inazalisha ufuta Dodoma ikiwemo, hivyo ni vyema viongozi wakaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu ubora wa mfumo huo.
Dk Mahenge alisema mfumo wa stakabadhi ghalani umepima faida mikoa mingi hasa ya kusini kuhusu korosho, baada ya kunyonywa na walanguzi kwa muda mrefu waliweka zao ghalani wakauza kwa mnada kwa bei kubwa na wakapata pesa na hadi wakanywesha mbuzi soda.
Alisema viongozi wanatakiwa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kupitia vyama vya ushirika kwamba mfumo wa stakabadhi ghalani ni mfumo bora ambao utawapa faida kubwa na hawapunjwa na walanguzi wanaowalalia bei.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
