Thursday, May 16, 2019
Watu 80 Wakamatwa Kwa Kula Mchana Wakati wa Ramadhan
Polisi wanaosimamia sheria ya kiislam (Sharia) katika jimbo la Kano nchini Nigeria wamewashikilia watu 80 kwa tuhuma za kula mchana hadharani, wakati wa mfungo wa Mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Polisi hao ambao wanafahamika kama Hisbah wameeleza kuwa watu hao walishikiliwa katika maeneo mbalimbali kwenye jiji la Kano ndani ya kipindi cha siku chache zilizopita.
Jimbo la Kano ni moja kati ya majimbo ya Kaskazini mwa Nigeria ambayo yanafuata sheria ya kidini (Sharia) tangu mwaka 2000, lakini wanazingatia pia sheria za nchi.
Msemaji wa Polisi wa Hisbah katika jimbo hilo, Adamu Yahaya ameiambia BBC kuwa watu hao waliokamatwa ni waumini wa dini ya Kiislam na kwamba maafisa wa jeshi hilo hawawakamati watu ambao sio waumini wa dini hiyo kwakuwa sheria za kiislam haziwahusu.
Alisema kuwa baadhi ya watu waliokamatwa waliwaambia maafisa wa polisi kuwa walikuwa wanakula kwa sababu wao binafsi hawakuuona mwezi ukiandama, na wengine walitoa sababu za ugonjwa ambazo zilionekana kuwa hazina mashiko.
Hata hivyo, Yahaya alisema kuwa watu hao wote 80 waliachiwa huru kwa sababu walibainika kuwa walifanya kosa hilo kwa mara ya kwanza.
Hisbah wameeleza kuwa wataendelea na msako wao katika kipindi chote cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na watawakamata waislamu wote ambao hawafuati masharti ya kufunga katika kipindi hiki bila kuwa na sababu za msingi.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
