TUZO za Mo Awards zilizoasisiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa klabu ya Simba, Mohammed Dewji zinatolewa leo Alhamisi ukiwa ni msimu wake wa pili. Tukio hilo la aina yake litafanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Regency na zitatolewa tuzo 12 kwa kikosi hicho cha Mabingwa wa Ligi Kuu Bara.
Hii itakuwa ni mara ya pili kwa tuzo hizo kutolewa baada ya mara ya kwanza mwaka jana.
Msimu huu tuzo hizo zitakuwa na mabadiliko tofauti na msimu uliopita baada ya vipengele kadhaa kuongezwa.
Tuzo hizo zitakuwa katika vipengele 12 ambavyo ni mchezaji bora wa mwaka, golikipa bora wa mwaka, goli bora la mwaka, beki bora wa mwaka, kiungo bora wa mwaka na mshambuliaji bora wa mwaka mchezaji mwenye umri mdogo, mchezaji bora wa kike na nyingine.
Hata hivyo tuzo hizo zilikuwa zinapigiwa kura katika kurasa tofauti za mitandao ya kijamii ya klabu ya Simba. Wachezaji ambao walipata tuzo hizo msimu uliopita ni pamoja na Aisha Manula, Erasto Nyoni, Shiza Kichuya, Emmanuel Okwi kwa Simba Queens alikuwa Zainabu Rashid. Kwa upande wake, Mohammed Dewji amesema kuwa tuzo za mwaka huu zitakuwa na hadhi kubwa zaidi tofauti ya zile za mwaka uliopita kutokana na maandalizi ambayo yamefanyika.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
