TUZO za Mo Awards zilizoasisiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa klabu ya Simba, Mohammed Dewji zinatolewa leo Alhamisi ukiwa ni msimu wake wa pili. Tukio hilo la aina yake litafanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Regency na zitatolewa tuzo 12 kwa kikosi hicho cha Mabingwa wa Ligi Kuu Bara.
Hii itakuwa ni mara ya pili kwa tuzo hizo kutolewa baada ya mara ya kwanza mwaka jana.
Msimu huu tuzo hizo zitakuwa na mabadiliko tofauti na msimu uliopita baada ya vipengele kadhaa kuongezwa.
Tuzo hizo zitakuwa katika vipengele 12 ambavyo ni mchezaji bora wa mwaka, golikipa bora wa mwaka, goli bora la mwaka, beki bora wa mwaka, kiungo bora wa mwaka na mshambuliaji bora wa mwaka mchezaji mwenye umri mdogo, mchezaji bora wa kike na nyingine.
Hata hivyo tuzo hizo zilikuwa zinapigiwa kura katika kurasa tofauti za mitandao ya kijamii ya klabu ya Simba. Wachezaji ambao walipata tuzo hizo msimu uliopita ni pamoja na Aisha Manula, Erasto Nyoni, Shiza Kichuya, Emmanuel Okwi kwa Simba Queens alikuwa Zainabu Rashid. Kwa upande wake, Mohammed Dewji amesema kuwa tuzo za mwaka huu zitakuwa na hadhi kubwa zaidi tofauti ya zile za mwaka uliopita kutokana na maandalizi ambayo yamefanyika.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...