Thursday, May 16, 2019
TRA Tarime wapokea maombi 152 ya msamaha wa kodi ya majengo
Na Timothy Itembe-Mara
Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Wilaya Tarime mkoani Mara kwa kuzingatia sheria ya Mamlaka ya mapato Tanzania namba 9 sura ya 399 sheria ya kodi ya majengo namba 2 sura ya 289 na sheria ya fedha ya serikali za mitaa namba 9 sura ya 290 wamepokea maombia 152 ya msamaha wa kodi kwa wazee na walemavuili kuyafanyia kazi.
Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake meneja TRA Wilaya Tarime mkoani hapa, Frank Lwesya alisema kuwa Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA)ina jukumu la kusimamia na kukusanya kodi ya majengo kwa hali hiyo wamepokea maombi 152 kutoka kwa wazee ili kuyafanyia kazi kwa mwaka wa fedha 2019.
"Majengo yaliyosamehewa na serikali kulipa kodi ya majengo kwa mujibu wa sheria ni pamoja na Nyumba moja ambayo inapaswa kulipiwa kodi ya majengo ambayo inamilikiwa na kuishi na Mtu mwenye umri wa zaidi ya miaka sitini (60) au Nyumba anayoishi mlemavu ambaye hana kipato chochote ambapo TRA Tarime tumepokea maombi 152 kati yao maombi 2 yamefanyiwa kazi na wamiliki wamesamehewa kodi ya majengo huku maombi mengine yanafanyiwa kazi"alisema Lwesya
Kwa upande wake Afisa Kodi TRA Wilaya Tarime,Taiboye Mwita alisema kuwa maombi hayo ni ya kila mwaka kwa kuzingatia sheria ya mamlaka ya mapato Tanzania TRA inayowataka wamiliki kutuma maombi kwa kila mwaka ili kufanyiwa tadhimini na maafisa wa TRA kuhakiki umiliki kwa kila muombaji.
Mwita aliongeza kuwa Mamlaka hiyo inafanya hivyo ili kuepuka mgongano na wamiliki wa Nyumba kubadilika kila mwaka ambapo katika tadhimini wanawatumia wenyeviti wa mitaa,Vitongoji na wale wa serikali za vijiji pamoja ma watendaji wao ili kupata uhakika zaidi na endapo mmiliki hana nyumba ya pili na nyumba ya biashara anapaswa kusamehewa kodi kama serikali ilivyoelekeza.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
