Sunday, May 5, 2019
Polisi Songwe: Hatuna taarifa za kukamatwa kwa Mdude Chadema
Polisi katika eneo la Songwe nyanda za juu kusini mwa Tanzania imesema kwa haina taarifa kuhusu tukio la kukamatwa kwa kijana Mdude Nyangali maarufu Mdude Chadema anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana siku ya jumamosi.
Tukio hilo limeendelea kuzua gumzo katika mitandao ya kijamii ndani na nje ya nchi hiyo huku wanaharakati wa kutetea haki wakianzisha kampeini ya kutaka kijana huyo achiwe huru.
Huku Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, George Kyando amesema kuwa ''hajazipata'' taarifa ya kukamatwa kijana huyo.
''Baada ya kuendelea kupokea na kufanyia kazi taarifa mbalimbali, kuhusu tukio hilo la Mdude, Chama kitazungumza na vyombo vya habari vya kitaifa na kimataifa kuhusu suala hili, siku ya Jumatatu, Mei 6, mwaka huu, ili kupaza sauti kubwa dhidi ya tukio hili na mengine ya namna hiyo yanayohusu utekwaji na upotezwaji wa wananchi katika mazingira yenye utata unaoibua maswali yanayotakiwa kujibiwa na mamlaka au vyombo vilivyopewa dhamana ya Kikatiba na kisheria kuhakikisha uhai wa raia ni jukumu namba moja kwa Serikali yoyote iliyoko madarakani.''
Chama hicho pia kimevitaka vyombo vya dola, hususan Jeshi la Polisi lenye wajibu wa kulinda raia na mali zao, kufuatilia taarifa za tukio hilo kama zilivyoripotiwa kwa polisi katika eneo husika na kuhakikisha Mdude anapatikana na wahalifu waliotenda tukio hilo wanajulikana, kukamatwa na kufikishwa mbele ya sheria.
Taarifa za awali kutoka kwa watu waliyoshuhudia tukio hilo zimedai kuwa baada ya kusikika kwa purukushani na kelelekatika duka la Mdude Chadema, baadhi ya wananchi walijitokeza kutaka kujua kilichokuwa kikiendelea ili kutoa msaada, lakini ghafla watu waliokuwa wakimpiga Mdude walitoa silaha aina ya bastola na kuwatishia wananchi hao, kitendo kilichowaogofya wananchi na kukimbia kwa hofu.
Imedaiwa kuwa watu hao walimuingiza Mdude kwenye 'buti' ya mojawapo ya gari hizo, wakamuachia yule kijana mwingine kisha wakaondoka na Mdude kuelekea kusikojulikana.
Madai ambayo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, George Kyando amekanusha katika mahojiano yake na Gazeti la Mwananchi nchini Tanzania
"Mimi ni mkazi wa eneo linalodaiwa kuwa risasi zimepigwa lakini sijasikia na kama unavyojua mji wa Vwawa ni mdogo ambao zikipigwa risasi lazima utasikia," alisema.
Hata hivyo, Kamanda Kyando amesema ataendelea kufuatilia kwa kina zaidi juu ya taarifa hizo.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
