Unapenda wimbo gani kutoka kwa mwanamziki Miriam Makeba? Binafsi huwa napenda nyimbo mbili kutoka kwa kwake ambazo ni malaika na hapo zamani japo mwanamziki huyu anazo nyimbo nyingi nyingi kama vile samba, pata pata na nyinginezo nyingi.
Mwanamziki Miriam Makeba alizaliwa tarehe 4 Machi 1932 katika jiji la Johannesburg huko Afrika Kusini. Mama yake alikuwa wa kabila la Swazi sangoma na baba yake wa kabila la Xhosa. Baba alifariki wakati Miriam akiwa na umri wa miaka sita.
Miriam alikuwa mwanamuziki pekee wakati huo aliyeweza kufanikiwa kuzieneza nyimbo zenye asili ya Kiafrika. Pia alikuwa miongoni mwa wanamuziki waasisi wa kuchanganya mitindo tofauti ya muziki na kutengeneza muziki wa kuvutia kama Kwaito.
Alianza kazi ya muziki mwanzoni mwa mwaka 1950 akiwa na kundi la The Skylarks, baadaye alijiunga na kundi la Manhattan Brothers. Makundi hayo yalikuwa yakipiga muziki wa Jazz wenye vionjo vya Kiafrika kusini.
Mwaka 1959, Miriam alifanya onyesho kubwa pamoja na Hugh Masekela maybe alikuja kuwa mume. Maonyesho aliyofanya pamoja na albamu nzuri alizorekodi havikumpatia faida, lakini baadaye alifanya matamasha katika nchi za Ulaya na Amerika.
Ulipoanza mkakati wa kupinga ubaguzi wa rangi uliokuwa ukiendelea Afrika ya kusini, Miriam aliamua kurudi nyumbani kupigania uhuru. Baadaye alialikwa Italia katika tamasha la filamu la Venice.
Kati ya nyimbo za Miriam zilizo maarufu ni Patapata (kwa lugha ya KiXhosa ni "Qongaqothwan"). Wimbo maarufu wa Malaika uliotungwa na Fadhili William Miriam aliuimba akishirikiana na Harry Belafonte.
Miriam alirudi tena nyumbani mwaka 1990, na mwaka 1992 alicheza filamu ya Sarafina.
Mwaka 2001 alitunukiwa tuzo ya dhahabu iliyoitwa Otto Hahn Peace Medal, pia alishika nafasi ya 38 kati ya wanamuziki bora kati ya 100 waliopewa tuzo nchini Afrika ya Kusini.
Mwaka wa 2005, Miriam alifanya ziara ya kimuziki kwa ajili ya kuwaaga marafiki wake wote duniani iliyomchukua miezi kumi na minne; alifanya maonyesho katika nchi zote alizotembelea wakati alipokuwa akifanya kazi ya muziki.
Aliaga dunia kwa shtuko la moyo alfajiri ya tarehe 10 Novemba 2008, nchini Italia baada ya kutoa onyesho la muziki.
Source
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
