Unapenda wimbo gani kutoka kwa mwanamziki Miriam Makeba? Binafsi huwa napenda nyimbo mbili kutoka kwa kwake ambazo ni malaika na hapo zamani japo mwanamziki huyu anazo nyimbo nyingi nyingi kama vile samba, pata pata na nyinginezo nyingi.
Mwanamziki Miriam Makeba alizaliwa tarehe 4 Machi 1932 katika jiji la Johannesburg huko Afrika Kusini. Mama yake alikuwa wa kabila la Swazi sangoma na baba yake wa kabila la Xhosa. Baba alifariki wakati Miriam akiwa na umri wa miaka sita.
Miriam alikuwa mwanamuziki pekee wakati huo aliyeweza kufanikiwa kuzieneza nyimbo zenye asili ya Kiafrika. Pia alikuwa miongoni mwa wanamuziki waasisi wa kuchanganya mitindo tofauti ya muziki na kutengeneza muziki wa kuvutia kama Kwaito.
Alianza kazi ya muziki mwanzoni mwa mwaka 1950 akiwa na kundi la The Skylarks, baadaye alijiunga na kundi la Manhattan Brothers. Makundi hayo yalikuwa yakipiga muziki wa Jazz wenye vionjo vya Kiafrika kusini.
Mwaka 1959, Miriam alifanya onyesho kubwa pamoja na Hugh Masekela maybe alikuja kuwa mume. Maonyesho aliyofanya pamoja na albamu nzuri alizorekodi havikumpatia faida, lakini baadaye alifanya matamasha katika nchi za Ulaya na Amerika.
Ulipoanza mkakati wa kupinga ubaguzi wa rangi uliokuwa ukiendelea Afrika ya kusini, Miriam aliamua kurudi nyumbani kupigania uhuru. Baadaye alialikwa Italia katika tamasha la filamu la Venice.
Kati ya nyimbo za Miriam zilizo maarufu ni Patapata (kwa lugha ya KiXhosa ni "Qongaqothwan"). Wimbo maarufu wa Malaika uliotungwa na Fadhili William Miriam aliuimba akishirikiana na Harry Belafonte.
Miriam alirudi tena nyumbani mwaka 1990, na mwaka 1992 alicheza filamu ya Sarafina.
Mwaka 2001 alitunukiwa tuzo ya dhahabu iliyoitwa Otto Hahn Peace Medal, pia alishika nafasi ya 38 kati ya wanamuziki bora kati ya 100 waliopewa tuzo nchini Afrika ya Kusini.
Mwaka wa 2005, Miriam alifanya ziara ya kimuziki kwa ajili ya kuwaaga marafiki wake wote duniani iliyomchukua miezi kumi na minne; alifanya maonyesho katika nchi zote alizotembelea wakati alipokuwa akifanya kazi ya muziki.
Aliaga dunia kwa shtuko la moyo alfajiri ya tarehe 10 Novemba 2008, nchini Italia baada ya kutoa onyesho la muziki.
Source
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...