Sunday, May 5, 2019
Anusurika kuuwawa na Simba
Na Ahmad Mmow, Lindi.
Mtu mmoja anayetambulika kwa jina la Kizito Matei (59), mkazi wa kijiji na kata ya Rutamba, tarafa ya Rondo, wilaya na mkoa wa Lindi. Juzi usiku alinusurika kuuwawa na kuliwa na Simba.
Imeelezwa kwamba Kizito ambaye alijeruhiwa kwenye tukio hilo na amelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Lindi( Sokoine) alikutwa na mkasa huo majira ya saa tano usiku katika kitongoji cha Namatili.
Mdogo wake Kizito anaetambulika kwa jina la Michael alisema Kizito alipokuwa anarudi nyumbani kwake toka matembezini alipoona giza ni nene, na maeneo hayo yanawanyama wakali aliamua kuingia na kulala kwenye kibanda cha mgahawa ambacho kilikuwa hakijagandikwa.
" Simba walikuwa wawili, walikuwa wanamfukuza mbwa. Walipofika kwenye kibanda waligundua kulikuwa na mtu.Kwakuwa kilikuwa hakijagandikwa walimuona. Ndipo mmoja alipotaka amchomoe baada ya kupenyeza mkono kwenye mojawapo ya matundu," alisema Michael.
Ndugu huyo wa Kizito alisema kutokana na kitendo cha Simba huyo kutaka kumchomoa kwa nguvu kaka yake, ndipo alipomjeruhi maeneo mbalimbali ya mwili, hasa mkononi.
Alipoulizwa kaka yake aliwezaje kuokoka na kunusurika kufa kwenye tukio hilo. Alisema baada ya kuchomwa na makucha aliamka kutoka usingizi na kupiga kelele. Ndipo watu walipokwenda kwenye eneo la tukio. Jambo ambalo lilisababisha Simba hao wakimbie na kutokomea kusikojulikana.
Maelezo yote ya Michael yaliungwa mkono na Kizito mwenyewe ambae kwa mujibu wa mmoja wa maofisa waandamizi wa hospitali ya Sokoine, Dkt Ernest Mhando anaendelea kutibiwa na hali yake inaendelea vizuri.
Dkt Mhando alithibitisha kwamba Kizito alipokelewa katika hosipitali hiyo akiwa amejeruhiwa,hasa mkononi. Hata hivyo hali yake inaendelea vizuri na anaendelea kutibiwa.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
