TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), imewataka wadau wote wa michezo akiwemo Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera kuwasilisha malalamiko yao licha ya taasisi hiyo kuwatuma maofisa wake kufuatilia yanayoendelea kwenye Ligi Kuu Bara.
Takukuru wametoa kauli hiyo kufuatia hivi sasa wadau wengi wa soka kulalamika juu ya uwepo wa rushwa michezoni katika kuzihujumu timu kwenye mechi za mwisho za Ligi Kuu Bara. Zahera mara kwa mara amekuwa akilalamika juu ya baadhi ya timu kutumia vibaya fedha zao katika kuzihujumu timu nyingine.
Akizungumza na Championi Jumamosi, Naibu Mkurugenzi wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo, alisema kuwa kwa upande wao tayari vijana wao wapo kazini kufuatilia kila kitu kinachotokea katika ligi kuu kupitia timu shiriki huku akiwataka wadau akiwemo Zahera kuwapelekea malalamiko yao ili waweze kuyafanyia kazi.
"Ni kweli hizo taarifa zimetufikia lakini kitu kinachotusikitisha sana kutoka kwa wananchi (wadau) ni kwamba mambo yanaongelewa na watu lakini wahusika wanaoguswa na hayo mambo hawaji kutupa taarifa kwa ufasaha yaani kutupa kamili, nini kimetokea, nani kafanya nini wakati gani na wapi.
"Sasa tuna taarifa lakini ni za kuungaunga mno, sisi tungependa hao watu wanaolalamika waje watueleze, nani kachukua rushwa, wakati gani na wapi, sisi tunaingia kazini yaani tupo tayari, tumepata habari nusunusu vijana wetu wemekwenda kufanya uchunguzi lakini inakuwa vyema kama tunapata taarifa ambazo zimejitosheleza kwa sababu inatusaidia kuanza na tatizo kuliko kusubiria," alisema Mbungo.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...