Klabu ya Simba imewasili salama mjini Morogoro tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Mbao FC wikiendi hii.
Simba ambayo imetoka asubuhi ya leo jijini Dar es salaam na kuwasili Morogoro majira ya mchana, imepokelewa na mamia ya mashabiki katika hoteli waliyofikia ambao muda wote wameonekana kutaja majina ya wachezaji.
Jina la mshambuliaji John Bocco ndilo lilliloibua shangwe kubwa zaidi baada ya kushuka kutoka kwenye basi, ikionesha kuwa mashabiki wamekubali kiwango alichokionesha katika mechi mbili kubwa na muhimu za mwisho.
Mechi hizo ni ili iliyoipeleka Simba robo fainali ya Klabu Bingwa Afrika baada ya kuifunga AS Vita mabao 2-1 katika Uwanja wa Taifa pamoja na mechi iliyoipeleka Taifa Stars kwenye fainali za AFCON kwa kuichapa Uganda kwa mabao 3-0, ambapo katika mechi zote mshambuliaji huyo ameonesha kiwango kikubwa.
Makamanda wetu walivyopokelewa mji kasoro bahari (Morogoro). Siku ya Jumapili watakuwa uwanja wa Jamhuri kuwapa burudani Wanasimba wote. #NguvuMoja pic.twitter.com/ziQwF7cSni
— Simba Sports Club (@SimbaSCTanzania) March 29, 2019
Mabingwa hao watetezi wa ligi kuu wanatarajia kupambana na Mbao FC katika Uwanja wa Jamhuri kutokana na Uwanja wa Taifa kuwa katika maandalizi ya michezo ya AFCON ya vijana chini ya miaka 17 inayoratajia kuanza mwezi ujao nchini Tanzania.
Nafasi ya Simba katika msimamo wa ligi
Katika msimamo wa Ligi Kuu, Simba inakamata nafasi ya tatu ikiwa na pointi 54 baada ya kushuka dimbani michezo 21 huku Mbao FC ikiwa katika nafasi ya 14 kwa pointi 36 baada ya kushuka dimbani michezo 30.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
