Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ameipongeza timu ya soka ya taifa, Taifa Stars kwa kuifunga Uganda na kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika Afcon 2019.
Stars imefuzu fainali hizo kwa mara ya kwanza baada ya miaka 39 kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Uganda kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam juzi.
Katika salamu zake hizo za pongezi, Rais Shein alisema wananchi wa Zanzibar na Tanzania nzima wamefarijika na ushindi huo ambao utaendelea kuipa hadhi kubwa Tanzania Kitaifa na Kimataifa katika anga za michezo.
Alieleza kuwa wananchi wa Zanzibar na Tanzania nzima wataendelea kuiunga mkono Timu yao hiyo kutokana na jitihada kubwa inazozichukua katika kuhakikisha inailetea ushindi Tanzania.
Aidha, Rais Shein alitumia fursa hiyo kuwapongeza wananchi wote kwa kuishangilia timu yao.
Alilipongeza Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Kocha mkuu wa Stars, Emmanuel Amunike, watendaji na viongozi wote waliofanikisha ushindi huo kwa kuonesha kiwango cha hali ya juu.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...