Wednesday, March 27, 2019
BREAKING: Lukumay na Nyika wajiengua Yanga SC
Kaimu Mwenyekiti Yanga SC Samuel Lukumay na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Hussein Nyika wametangaza kujiuzulu nafasi zao.
Wawili hao wameamua kuachia ngazi mapema ili kupisha mchakato wa uchaguzi mkuu wa klabu ambao utafanyika hivi karibuni.
Nyika na Lukumay wameamua kujiondoa ili kutoa mwanya mzuri kwa mchakato wa uchaguzi kwenda vizuri ili kuja kupata warithi wa nafasi hizo.
Licha ya kujiuzulu, Nyika amewamba msamaha wale wote aliowakosea pindi akiwa madarakani ndani ya klabu.
''Ninajiuzulu nafasi zangu zote nikiwa kama Mjumbe wa kamati ya utendaji.
"Lakini pia Mwenyekiti wa kamati ya usajili na kamati ya mashindano na niombe msamaha kwa wale niliowakosea katika utekelezaji wangu wa majukumu''.
Ikumbukwe hivi karibuni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Yanga, George Mkuchika, alitangaza kuwa watakuwa na mkutano mkuu maalum utakaoenda kuamua kama klabu inahitaji kufanya uchaguzi mkuu ama wa kujaza nafasi.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...