Familia moja kutoka kijiji cha Lubai, Kaunti ya Kakamega nchini Kenya imelazimisha kijana wao wa kiume kuzika mgomba wa ndizi ili kuashiria mwili wa mke wake ambaye alitoweka miaka 13 iliyopita.
Bernard Munase alishawishiwa na wazee wa jamii ya Waisukha kufanya sherehe za kumzika mkewe kulingana na tamaduni za jamii hiyo ili aweze kuoa mke mwingine.
Wazee wa jamii hiyo wamesema walihitajika kufanya sherehe ili kumpa fursa kijana wao kuoa mke mwingine. Munase amesema amemtafuta mkewe kila pembe bila mafanikio na sasa hana imani tena iwapo atampata akiwa hai.
"Mungu alikuwa ametubariki na mtoto wa kiume kabla mke wangu kujatoweka, mimi pamoja na jamaa zangu tumemtafuta kila mahali bila mafanikio", amesema Munase.
Baada ya sherehe hiyo, wazee hao wa jadi wamesema Munase sasa yuko huru kuoa mke mwingine huku wakiamini yule wa awali aliaga dunia.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
