Sunday, February 24, 2019
Ndege yatua kwa dharura baada ya jaribio la kuiteka nyara
Ndege iliyokuwa inafanya safari kutoka mji mkuu wa Bangladesh, Dhaka kuelekea Dubai, ililazimika kutua kwa dharura baada ya kutokea jaribio la kuteka nyara ndege, vyombo vya habari nchini humo vimeripoti.
Ndege ya shirika la Binman, ikiwa na abiria 142, ilizungukwa na vikosi vya usalama katika uwanja wa ndege wa mji wa pwani wa Chittagong.
Abiria wa ndege BG 147 walitoka ndani ya ndege hiyo wakiwa salama, ripoti zilieleza zikinukuu polisi.
Mtu mmoja aliyekisiwa kujaribu kuvamia chumba cha rubani alikamatwa, Shirika la habari la Ufaransa limeeleza.
Ndege hiyo iliwekwa kwenye uangalizi mara moja ilipotua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Shah Amanat wakati polisi wakizungumza na mshukiwa huyo.
Picha zilizowekwa kwenye mitandao ya kijamii zilionyesha watu wakiwa katika makundi makundi huku ndege aina ya Boeing 737 ikionekana kwa nyuma.
Haijafahamika kwa nini mshukiwa huyo anayeaminika kuwa na umri wa miaka 25, alijaribu kuteka nyara ndege.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...