Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt. (Mst) George H. Mkuchika (Mb) ameahidi kuwachukulia hatua za kinidhamu watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale waliotumia vibaya fedha za miradi ya maendeleo na kupelekea kutomalizika kwa miradi hiyo.
Kauli hiyo ameitoa wilayani Liwale wakati wa kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale mkoani Lindi, kabla ya kutembelea utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na TASAF wilayani humo.
Mhe. Mkuchika amewataka watumishi wote wanaojijua kuhusika na ubadhirifu wa fedha za miradi ya maendeleo kuzirudisha mapema kabla majina yao hayajafikishwa ofisini kwake.
Mhe. Mkuchika amefafanua kuwa, Serikali imekuwa ikipeleka fedha za miradi ya maendeleo kila wilaya mkoani Lindi ili kutekeleza ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwezo zahanati, vituo vya afya, umwagiliaji na ujenzi wa barabara lakini fedha hizo zimeonekana kutumika vibaya kwani miradi haijamalizika lakini fedha zimeisha.
Mhe. Mkuchika ameainisha kuwa, taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale inaonyesha Halmashauri hiyo inadaiwa takribani shilingi milioni 465 hivyo kupelekea kuzorota kwa uchumi wa Wilaya hiyo kutokana na makusanyo ya fedha kuishia kulipa madeni yanayotokana na matumizi mabaya ya fedha.
Mhe. Mkuchika amesema, amechoshwa na barua za malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusiana na matumizi mabaya ya fedha zinazotolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya wilayani humo.
Aidha, Mhe. Mkuchika amewataka watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Liwale kuridhika na mishahara yao na kuacha kuomba rushwa kutoka kwa wananchi wanapohitaji huduma kwani kwa kufanya hivyo, kunawanyima wananchi haki yao ya kupata huduma.
Mhe. Mkuchika amefafanua kuwa rushwa ni adui wa haki na kutoa angalizo kuwa nchi ambazo rushwa imekithiri, mwenye haki ni mtu mwenye fedha kwa kuwa kila sehemu ataweza kushinda kwa kutoa fedha zake.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) yuko katika ziara ya kikazi mkoani Lindi yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi kwa umma, ikiwa ni pamoja na kukagua na kujiridhisha na utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na TASAF mkoani humo.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
