Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt. (Mst) George H. Mkuchika (Mb) ameahidi kuwachukulia hatua za kinidhamu watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale waliotumia vibaya fedha za miradi ya maendeleo na kupelekea kutomalizika kwa miradi hiyo.
Kauli hiyo ameitoa wilayani Liwale wakati wa kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale mkoani Lindi, kabla ya kutembelea utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na TASAF wilayani humo.
Mhe. Mkuchika amewataka watumishi wote wanaojijua kuhusika na ubadhirifu wa fedha za miradi ya maendeleo kuzirudisha mapema kabla majina yao hayajafikishwa ofisini kwake.
Mhe. Mkuchika amefafanua kuwa, Serikali imekuwa ikipeleka fedha za miradi ya maendeleo kila wilaya mkoani Lindi ili kutekeleza ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwezo zahanati, vituo vya afya, umwagiliaji na ujenzi wa barabara lakini fedha hizo zimeonekana kutumika vibaya kwani miradi haijamalizika lakini fedha zimeisha.
Mhe. Mkuchika ameainisha kuwa, taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale inaonyesha Halmashauri hiyo inadaiwa takribani shilingi milioni 465 hivyo kupelekea kuzorota kwa uchumi wa Wilaya hiyo kutokana na makusanyo ya fedha kuishia kulipa madeni yanayotokana na matumizi mabaya ya fedha.
Mhe. Mkuchika amesema, amechoshwa na barua za malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusiana na matumizi mabaya ya fedha zinazotolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya wilayani humo.
Aidha, Mhe. Mkuchika amewataka watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Liwale kuridhika na mishahara yao na kuacha kuomba rushwa kutoka kwa wananchi wanapohitaji huduma kwani kwa kufanya hivyo, kunawanyima wananchi haki yao ya kupata huduma.
Mhe. Mkuchika amefafanua kuwa rushwa ni adui wa haki na kutoa angalizo kuwa nchi ambazo rushwa imekithiri, mwenye haki ni mtu mwenye fedha kwa kuwa kila sehemu ataweza kushinda kwa kutoa fedha zake.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) yuko katika ziara ya kikazi mkoani Lindi yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi kwa umma, ikiwa ni pamoja na kukagua na kujiridhisha na utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na TASAF mkoani humo.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...