Chama cha Soka cha Misri (EFA) kimetangaza kuwa kimehakikishiwa ulinzi kwa mashabiki wasiozidi 10,000 ambao watahudhuria mchezo wa Al Ahly dhidi ya Simba, kesho Jumamosi katika Ligi ya Mabingwa Afrika.
Al Ahly inaongoza Kundi D katika michuano hiyo ikiwa na pointi nne wakati Simba inashika nafasi ya tatu kwa kuwa na pointi tatu.
Timu hizo zinatarajiwa kukutana kwenye Uwanja wa Borg El Arab unaoingiza watu 80,000 waliokaa kwenye siti.
Taarifa hizo zimekuja baada ya kutolewa tetesi juu ya idadi ya mashabiki ambao wanatakiwa kuingia uwanjani, hivyo Al Ahly wametakiwa kutoa idadi hiyo ya tiketi ili kukwepa adhabu kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kutokana na suala la kiusalama.
Mwamuzi wa mchezo huo anatarajiwa kuwa Maguette Ndiaye raia wa Senegal na atasaidiwa na Djibril Camara pamoja na El Hadji Malick Samba, wakati ofisa wa nne ni Daouda Gueye.
Siku chache zilizopita, Caf ilitangaza kuiondoa Ismaily ya Misri katika michuano hiyo kutokana na mashabiki wao kuonyesha utovu wa nidhamu uliovuka mipaka ikiwemo kurusha mawe uwanjani, chupa za maji, kwa mwamuzi wa akiba na kwa mashabiki wageni katika mchezo wa timu hiyo dhidi ya Club Africain, Januari 18, mwaka huu.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
