Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani Iringa kimesema mbunge wa chama hicho Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amezuiwa na polisi kufanya mkutano wa hadhara katika viwanja vya Mwembetogwa.
Katibu wa Chadema Mkoa wa Iringa, Jackson Mnyawami amesema mkutano huo ulikuwa ufanyike leo, kwamba wamepokea barua ya polisi ikiwataka wasiendelee na mkutano huo.
Barua ya Novemba 21, 2018 iliyotolewa na mkuu wa polisi Wilaya ya Iringa kwenda kwa mbunge huyo inaeleza kuwa mkutano huo umezuiwa kutokana na taarifa za kiintelejensia.
"Polisi Iringa tunazo taarifa kuna kikundi cha watu wanaojiandaa kufanya fujo katika mkutano huo. Hali hiyo inaweza kuleta uvunjifu mkubwa wa amani," inaeleza sehemu ya barua hiyo.
"Hakuna askari wa kutosha kwa ajili ya kusimamia mkutano huo kwani nguvu kazi kubwa imeelekezwa katika shughuli maalum za kitaifa ya usimamizi wa mitihani ya kidato cha nne, cha pili na darasa la nne."
Mnyawani amesema wameipokea barua hiyo ya polisi ikiwa na sababu mbalimbali.
"Sababu tulizoelezwa ni za kiintelejensia kwamba kuna watu watafanya vurugu lakini pia wamesema kuwa kuna shughuli za kitaifa, ikiwa ni pamoja na mitihani inayoendelea kufanywa na wanafunzi wa kidato cha nne," amesema.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
