Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mh, Jokate Mwegelo amemsaidia mama aliyejifungua watoto mapacha waliyo ungana maini kupata bima ya afya na nyumba bora ya kuishi kutoka UBA United Bank for Africa hii inakuja mara baada ya mama huyo pamoja na watoto wake kupata ruksa ya kurejea nyumbani kwao Kisarawe.
Mama huyo wa watoto mapacha Gracious na Precious Michael Mkono wamepata ruksa rasmi katika Hospitali ya Muhimbili mara baada ya kufika hapo toka tarehe 21/07/2018 kupata matibabu baada ya kujifungulia nyumbani.
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), imefanikiwa kufanya upasuaji huo wa kuwatenganisha mapacha hao walioungana wakiwa chini ya miaka mitatu, ambao wamezaliwa Kisarawe mkoani Pwani, Julai 12, mwaka huu. Jumatano ya Septemba 26, Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Profesa Laurence Moselu, alisema upasuaji huo uliofanyika Septemba 23, kwa mafanikio makubwa ilienda vizuri.
Kwa mujibu wa Daktari bingwa wa upasuaji kwa watoto Dkt. Petronila Ngiloi amesema mapacha hao walizaliwa na mama yao aitwaye Esta (22) nyumbani kwao Kisarawe, alikozalishwa nyumbani baada ya kugundua watoto wameungana walipelekwa Kituo cha Afya cha Kibaha na baadaye kuhamishiwa Muhimbili wakiwa wamechoka sana.
Amesema watoto hao walipochunguzwa iligundulika wameungana sehemu kubwa ya ini na ikaonekana upasuaji huo unaweza kufanyika MNH ambapo walifanya kazi ili kuona mama huyo anapata huduma nzuri
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Geneva, Switzerland /AFP /.More than 100 groups urged the International Labour Organization to stop taking money from tobacco companies as t...