Wazee wa kimila na waganga wa jadi wilayani Nzega wameendesha kongamano la kimila kumuombea Mbunge wao ambaye Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt Hamisi Kigwangala huku wakitoa onyo kwa wanasiasa wanaomendea nafasi yake.
Wazee hao kwa pamoja wametoa kauli hiyo hii leo katika dua maalum ya kimila ya kumuombea Mbunge wao iliyofanyika wilayani humo ikiwa ni siku chache baada ya kiongozi huyo kuruhusiwa hospitali kufuatia ajali mbaya ya gari.
Aidha katika kuwashukuru wananchi wa wilaya hiyo, Waziri Kigwangala kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika,
"Hakuna maombi ama dua ambazo sikupokea jimboni siku hizi nne nilizofika kwa mara ya kwanza toka nisalimike kwenye ajali. Ahsanteni sana ndugu zangu kwa upendo na mshkamano mlionionesha".
"Mmenipa nyongeza kubwa sana ya deni kwenu. Nawaahidi kupambania Nzega yetu kwa nguvu zaidi!", ameongeza.
Hatua hiyo imekuja baada ya wananchi wa Nzega kumuomba kiongozi huyo awatembelee kwaajili ya dua pamoja na kuwashukuru kufuatia ajali ya gari ambayo aliipata, Agosti 4 mwaka huu katika kijiji cha Magugu Mkoani Manyara baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kupinduka na kupelekea kifo cha aliyekuwa Afisa Habari wake Hamza Temba.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
