Wazee wa kimila na waganga wa jadi wilayani Nzega wameendesha kongamano la kimila kumuombea Mbunge wao ambaye Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt Hamisi Kigwangala huku wakitoa onyo kwa wanasiasa wanaomendea nafasi yake.
Wazee hao kwa pamoja wametoa kauli hiyo hii leo katika dua maalum ya kimila ya kumuombea Mbunge wao iliyofanyika wilayani humo ikiwa ni siku chache baada ya kiongozi huyo kuruhusiwa hospitali kufuatia ajali mbaya ya gari.
Aidha katika kuwashukuru wananchi wa wilaya hiyo, Waziri Kigwangala kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika,
"Hakuna maombi ama dua ambazo sikupokea jimboni siku hizi nne nilizofika kwa mara ya kwanza toka nisalimike kwenye ajali. Ahsanteni sana ndugu zangu kwa upendo na mshkamano mlionionesha".
"Mmenipa nyongeza kubwa sana ya deni kwenu. Nawaahidi kupambania Nzega yetu kwa nguvu zaidi!", ameongeza.
Hatua hiyo imekuja baada ya wananchi wa Nzega kumuomba kiongozi huyo awatembelee kwaajili ya dua pamoja na kuwashukuru kufuatia ajali ya gari ambayo aliipata, Agosti 4 mwaka huu katika kijiji cha Magugu Mkoani Manyara baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kupinduka na kupelekea kifo cha aliyekuwa Afisa Habari wake Hamza Temba.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
