Wazee wa kimila na waganga wa jadi wilayani Nzega wameendesha kongamano la kimila kumuombea Mbunge wao ambaye Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt Hamisi Kigwangala huku wakitoa onyo kwa wanasiasa wanaomendea nafasi yake.
Wazee hao kwa pamoja wametoa kauli hiyo hii leo katika dua maalum ya kimila ya kumuombea Mbunge wao iliyofanyika wilayani humo ikiwa ni siku chache baada ya kiongozi huyo kuruhusiwa hospitali kufuatia ajali mbaya ya gari.
Aidha katika kuwashukuru wananchi wa wilaya hiyo, Waziri Kigwangala kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika,
"Hakuna maombi ama dua ambazo sikupokea jimboni siku hizi nne nilizofika kwa mara ya kwanza toka nisalimike kwenye ajali. Ahsanteni sana ndugu zangu kwa upendo na mshkamano mlionionesha".
"Mmenipa nyongeza kubwa sana ya deni kwenu. Nawaahidi kupambania Nzega yetu kwa nguvu zaidi!", ameongeza.
Hatua hiyo imekuja baada ya wananchi wa Nzega kumuomba kiongozi huyo awatembelee kwaajili ya dua pamoja na kuwashukuru kufuatia ajali ya gari ambayo aliipata, Agosti 4 mwaka huu katika kijiji cha Magugu Mkoani Manyara baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kupinduka na kupelekea kifo cha aliyekuwa Afisa Habari wake Hamza Temba.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
