Monday, October 1, 2018
Spika Ndugai amuandikia barua Mwenyekiti wa NEC kujiuzulu kwa Mbunge wa Chadema
Kufuatia kujiuzulu ubunge wa Jimbo la Serengeti mkoani Mara, Marwa Ryoba Chacha, Spika wa Bunge, Job Ndugai amemuandikia barua Mwenyekiti wa Tume ye Uchaguzi NEC, Jaji Semistacles Kaijage kumfahamisha kuwa jimbo hilo kwa sasa lipo wazi.
Spika Ndugai ameandika barua hiyo kwa mujibu wa kifungu 37(3) cha sheria ya Taifa ya uchaguzi kinachoelekeza kwamba pale ambapo mbunge amejiuzulu, atafariki au ataacha kazi ya ubunge kwa sababu nyingine yoyote tofauti na zilizoainishwa katika kifungu cha 113 cha sheria hiyo, Spika atamjulisha Mwenyekiti wa NEC na kutangaza kwenye gazeti la Serikali kwamba kiti hicho kiko wazi.
Chacha alitangaza kujiuzulu Ubunge na nafasi zake zote za uongozi ndani ya Chadema huku akitangaza kujiunga na Chama cha Mapinduzi kwa kile alichoeleza kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli katika kuwatumikia wananchi wa Tanzania.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...