Monday, October 1, 2018
Spika Ndugai amuandikia barua Mwenyekiti wa NEC kujiuzulu kwa Mbunge wa Chadema
Kufuatia kujiuzulu ubunge wa Jimbo la Serengeti mkoani Mara, Marwa Ryoba Chacha, Spika wa Bunge, Job Ndugai amemuandikia barua Mwenyekiti wa Tume ye Uchaguzi NEC, Jaji Semistacles Kaijage kumfahamisha kuwa jimbo hilo kwa sasa lipo wazi.
Spika Ndugai ameandika barua hiyo kwa mujibu wa kifungu 37(3) cha sheria ya Taifa ya uchaguzi kinachoelekeza kwamba pale ambapo mbunge amejiuzulu, atafariki au ataacha kazi ya ubunge kwa sababu nyingine yoyote tofauti na zilizoainishwa katika kifungu cha 113 cha sheria hiyo, Spika atamjulisha Mwenyekiti wa NEC na kutangaza kwenye gazeti la Serikali kwamba kiti hicho kiko wazi.
Chacha alitangaza kujiuzulu Ubunge na nafasi zake zote za uongozi ndani ya Chadema huku akitangaza kujiunga na Chama cha Mapinduzi kwa kile alichoeleza kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli katika kuwatumikia wananchi wa Tanzania.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...

