Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka nchini TFF imetangaza kuwa timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' itasafiri na ndege maalumu kuelekea nchini Cape Verde kwaajili ya mchezo wa kufuzu michuano ya AFCON.
Taifa Stars inatarajia kucheza na Cape Verde mjini Praia, 12 Oktoba kabla ya mchezo wa marudio utakaopigwa Jumanne 16, Oktoba jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na wanahabari kuhusiana na uamuzi huo, Waziri Dkt.Harrison Mwakyembe amesema,
" Mechi hizi mbili ni muhimu kwa sisi kushinda ili kujiweka katika mazingira ya kuzufu mwakani nchini Cameroon, tumeona njia pekee ni kutumia silaha yetu ya mwisho ambayo ni Boeng 787 Dreamliner, Asante JPM. Hii ni ndege pekee kwanza isiyochosha kwa safari ndefu na inayoweza kuibeba Taifa Stars na mashabiki wake bila kutua shemu yoyote ", amesema Dkt.Mwakyembe.
" Kwa Taifa Stars kutua nchi kama ile tena kwa Dreamliner ikishuka na wachezaji kama Mbwana Samatta, tayari tumeshawapiga bao mbili kisaikolojia ", ameongeza.
Pia Waziri Mwakyembe ametangaza bei kwa mashabiki wanaotaka kwenda kuisapoti timu yao, ambayo ni dola 1,500 ambazo ni sawa na Shilingi 3.5 millioni za Kitanzania kwa daraja la kawaida na dola 2,000 kwa daraja la kibiashara 'Business Class'.
Kwa upande wake, Rais wa TFF, Wallace Karia amewataka watanzania kujitokeza kuchangamkia fursa hiyo ya kuungana na timu yao katika ndege moja na wachezaji ili kwenda kuishangilia na kuhakikisha timu inarejea na matokeo mazuri.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
