Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka nchini TFF imetangaza kuwa timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' itasafiri na ndege maalumu kuelekea nchini Cape Verde kwaajili ya mchezo wa kufuzu michuano ya AFCON.
Taifa Stars inatarajia kucheza na Cape Verde mjini Praia, 12 Oktoba kabla ya mchezo wa marudio utakaopigwa Jumanne 16, Oktoba jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na wanahabari kuhusiana na uamuzi huo, Waziri Dkt.Harrison Mwakyembe amesema,
" Mechi hizi mbili ni muhimu kwa sisi kushinda ili kujiweka katika mazingira ya kuzufu mwakani nchini Cameroon, tumeona njia pekee ni kutumia silaha yetu ya mwisho ambayo ni Boeng 787 Dreamliner, Asante JPM. Hii ni ndege pekee kwanza isiyochosha kwa safari ndefu na inayoweza kuibeba Taifa Stars na mashabiki wake bila kutua shemu yoyote ", amesema Dkt.Mwakyembe.
" Kwa Taifa Stars kutua nchi kama ile tena kwa Dreamliner ikishuka na wachezaji kama Mbwana Samatta, tayari tumeshawapiga bao mbili kisaikolojia ", ameongeza.
Pia Waziri Mwakyembe ametangaza bei kwa mashabiki wanaotaka kwenda kuisapoti timu yao, ambayo ni dola 1,500 ambazo ni sawa na Shilingi 3.5 millioni za Kitanzania kwa daraja la kawaida na dola 2,000 kwa daraja la kibiashara 'Business Class'.
Kwa upande wake, Rais wa TFF, Wallace Karia amewataka watanzania kujitokeza kuchangamkia fursa hiyo ya kuungana na timu yao katika ndege moja na wachezaji ili kwenda kuishangilia na kuhakikisha timu inarejea na matokeo mazuri.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...