Klabu ya soka ya Yanga, huenda itawakosa nyota wake wawili kwenye mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara (TPL), Jumapili dhidi ya watani wao wa jadi Simba.
Kwa mujibu wa meneja wa kikosi hicho ambacho kimepiga kambi mkoani Morogoro, Nadir Haroub Cannavaro, wachezaji Juma Mahadhi na Juma Abdul hali zao bado si nzuri.
''Kambi inaendelea vizuri hapa Morogoro na wachezaji wote wapo tayari kwa mchezo isipokuwa beki wetu Juma Abdul na mshambuliaji Juma Mahadhi ambao bado ni majeruhi na hawapo tayari kwa mchezo wa Jumapili'', amesema Cannavaro.
Cannavaro ameeleza kukosekana kwa wachezaji hao hakutaathiri chochote kwani wachezaji waliopo wanauwezo wa kuipa timu matokeo kama ilivyokuwa kwenye mchezo dhidi ya Singida United ambapo walikosekana Kelvin Yondani, Mrisho Ngassa na Heritier Makambo, lakini timu ilipata ushindi.
Mchezo huo wa jumapili utakuwa wa tano kwa Yanga SC msimu huu, ambapo tayari wamecheza mechi 4 na kushinda zote. Wana alama 12 katika nafasi ya 3 ya msimamo wa ligi.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
