Klabu ya soka ya Yanga, huenda itawakosa nyota wake wawili kwenye mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara (TPL), Jumapili dhidi ya watani wao wa jadi Simba.
Kwa mujibu wa meneja wa kikosi hicho ambacho kimepiga kambi mkoani Morogoro, Nadir Haroub Cannavaro, wachezaji Juma Mahadhi na Juma Abdul hali zao bado si nzuri.
''Kambi inaendelea vizuri hapa Morogoro na wachezaji wote wapo tayari kwa mchezo isipokuwa beki wetu Juma Abdul na mshambuliaji Juma Mahadhi ambao bado ni majeruhi na hawapo tayari kwa mchezo wa Jumapili'', amesema Cannavaro.
Cannavaro ameeleza kukosekana kwa wachezaji hao hakutaathiri chochote kwani wachezaji waliopo wanauwezo wa kuipa timu matokeo kama ilivyokuwa kwenye mchezo dhidi ya Singida United ambapo walikosekana Kelvin Yondani, Mrisho Ngassa na Heritier Makambo, lakini timu ilipata ushindi.
Mchezo huo wa jumapili utakuwa wa tano kwa Yanga SC msimu huu, ambapo tayari wamecheza mechi 4 na kushinda zote. Wana alama 12 katika nafasi ya 3 ya msimamo wa ligi.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...