Thursday, September 20, 2018
Mbowe atakiwa kuacha upotoshaji, NEC yatoa ushahidi wake
TUME ya Taifa ya Uchaguzi NEC imejibu tuhuma zilizotolewa dhidi yao na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuhusu kufukuzwa kwa mawakala wa chama hicho kwenye vituo vya uchaguzi mdogo wa jimbo la Monduli uliofanyika Septemba 16 mwaka huu akisema ni uongo na kwamba tume haitotishwa na tuhuma hizo.
Akijibu tuhumu hizo Mkurugenzi wa NEC, Dk Athuman Kihamia amesema siyo kweli kwamba walifukuzwa bali kilichotokea ni kwamba wapo mawakala walioenda kwenye vituo ambavyo siyo vyao huku wengine wakiwa hawajafika asubuhi ya uchaguzi hivyo Chadema wakateua mawakala wengine ambao walikuwa hawatambuliki.
" Nilikuwepo Monduli mimi na waliniomba niwasaidie kwa sababu mawakala wao walikamatwa na Polisi nilipowaambia twendeni nikawaone hawakuja wao walikuwa wanaongea kwa simu tu.
" Natoa ushahidi kituo cha Siditi I cha pili, wakala aliyeapa ni George Ole Ngalimo lakini aliyefika kituoni ni Bosco Lawrence, hii habari ndugu zangu haikubaliki na huu siyo mchezo wa kuigiza wakala asiyeapa hawezi kuwa wakala rasmi. Lakini kituo cha Zaburi moja na kituo cha Isimangoni Chadema hawakusimamisha kabisa hivyo wasingeweza kuruhusiwa na msimamizi," amesema Dk Kihamia.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
