Thursday, September 20, 2018
Mbowe atakiwa kuacha upotoshaji, NEC yatoa ushahidi wake
TUME ya Taifa ya Uchaguzi NEC imejibu tuhuma zilizotolewa dhidi yao na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuhusu kufukuzwa kwa mawakala wa chama hicho kwenye vituo vya uchaguzi mdogo wa jimbo la Monduli uliofanyika Septemba 16 mwaka huu akisema ni uongo na kwamba tume haitotishwa na tuhuma hizo.
Akijibu tuhumu hizo Mkurugenzi wa NEC, Dk Athuman Kihamia amesema siyo kweli kwamba walifukuzwa bali kilichotokea ni kwamba wapo mawakala walioenda kwenye vituo ambavyo siyo vyao huku wengine wakiwa hawajafika asubuhi ya uchaguzi hivyo Chadema wakateua mawakala wengine ambao walikuwa hawatambuliki.
" Nilikuwepo Monduli mimi na waliniomba niwasaidie kwa sababu mawakala wao walikamatwa na Polisi nilipowaambia twendeni nikawaone hawakuja wao walikuwa wanaongea kwa simu tu.
" Natoa ushahidi kituo cha Siditi I cha pili, wakala aliyeapa ni George Ole Ngalimo lakini aliyefika kituoni ni Bosco Lawrence, hii habari ndugu zangu haikubaliki na huu siyo mchezo wa kuigiza wakala asiyeapa hawezi kuwa wakala rasmi. Lakini kituo cha Zaburi moja na kituo cha Isimangoni Chadema hawakusimamisha kabisa hivyo wasingeweza kuruhusiwa na msimamizi," amesema Dk Kihamia.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...