Baada ya Simba kubaki jijini Dar na kuweka kambi katika Hoteli ya Sea Scape iliyopo Mbezi Beach, jana Jumatano kikosi hicho kilifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Boko.
Katika mazoezi hayo, uongozi wa Simba uliwawekea ulinzi mkali nyota wake hao kuelekea mchezo wao wa Jumapili dhidi ya Yanga utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.
Katika mazoezi hayo ya jana, licha ya mashabiki kuwepo hapo uwanjani lakini kulikuwa na makomandoo kadhaa ambao walikuwa wanazungu kazunguka wakati mazoezi yakiendelea.
Hata hivyo, katika mazoezi hayo, wachezaji wa Simba walionekana kufanyishwa mazoezi ya nguvu na makocha wa kikosi hicho.
Katika zoezi hilo, wachezaji walionekana wakipambana licha ya baadhi yao kulalamika kutokana na aina ya mazoezi ambayo walikuwa wanayafanya kuonekana ni ya nguvu.
Katika mazoezi hayo, Hassan Dilunga na Mzamiru Yassin ndiyo wachezaji ambao hawakufanya mazoezi na wenzao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ni majeruhi.
Katika mazoezi hayo, kocha msaidizi wa timu hiyo, Masoud Djuma alionekana uwanjani akiendelea na majukumu yake kama kawaida licha ya kwamba hapo awali hakusafiri na timu ilipokwenda kucheza mikoani ikiripotiwa kutokuwa na maelewano mazuri na wenzake wa benchi la ufundi.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
