Baada ya Simba kubaki jijini Dar na kuweka kambi katika Hoteli ya Sea Scape iliyopo Mbezi Beach, jana Jumatano kikosi hicho kilifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Boko.
Katika mazoezi hayo, uongozi wa Simba uliwawekea ulinzi mkali nyota wake hao kuelekea mchezo wao wa Jumapili dhidi ya Yanga utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.
Katika mazoezi hayo ya jana, licha ya mashabiki kuwepo hapo uwanjani lakini kulikuwa na makomandoo kadhaa ambao walikuwa wanazungu kazunguka wakati mazoezi yakiendelea.
Hata hivyo, katika mazoezi hayo, wachezaji wa Simba walionekana kufanyishwa mazoezi ya nguvu na makocha wa kikosi hicho.
Katika zoezi hilo, wachezaji walionekana wakipambana licha ya baadhi yao kulalamika kutokana na aina ya mazoezi ambayo walikuwa wanayafanya kuonekana ni ya nguvu.
Katika mazoezi hayo, Hassan Dilunga na Mzamiru Yassin ndiyo wachezaji ambao hawakufanya mazoezi na wenzao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ni majeruhi.
Katika mazoezi hayo, kocha msaidizi wa timu hiyo, Masoud Djuma alionekana uwanjani akiendelea na majukumu yake kama kawaida licha ya kwamba hapo awali hakusafiri na timu ilipokwenda kucheza mikoani ikiripotiwa kutokuwa na maelewano mazuri na wenzake wa benchi la ufundi.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...