Wednesday, September 12, 2018
Chadema yawataka wanaohama chama kumuiga Nyalandu
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo, CHADEMA, Dk. Vincent Mashinji, amesema, Wabunge na Madiwani wanaojiuzulu na kuhama chama, waondoke tu kwa wema wala hakuna haja ya kusuguana na kusumbuana kila kukicha.
Dk. Mashinji ameweka wazi hilo leo kwenye mkutano wake na wanahabari jijini Dar es salaam, ambapo amesisitiza kuwa, mtu kuhama chama ni kutekeleza haki yake ya msingi ya Kikatiba na sio jambo la kusubiri usiku wa saa 6:00 ndio utangaze.
''Kati ya Wabunge 73 tuliopata kwenye uchaguzi mkuu 2015, watatu ndio wamehama, lakini wanatangaza usiku wakati hakuna haja ya kufanya hivyo maana Mwenyekiti alishawaambia waondoke tu kwa wema na chama hakitahangaika nao'', amesema, Dk. Mashinji.
Aidha, Dk. Mashinji ameongeza kuwa wanaohama wangeiga mfano wa aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini kupitia (CCM), Lazaro Nyalandu, ambaye alijiuzulu nafasi yake kwa kufuata utaratibu ikiwemo kumwandikia barua Katibu wa chama chake pamoja na Spika wa Bunge.
Aidha, CHADEMA imewahakikishia wanachama wake kuwa, imejipanga vyema na ina uungwaji mkono mzuri katika majimbo mawili yanayofanya uchaguzi mdogo wa Wabunge ya Monduli na Ukonga na wanategemea kuibuka na ushindi.
Wabunge wa CHADEMA waliojiuzulu ni Godwin Mollel, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Siha Mkoani Kilimanjaro, Mwita Mwikwabe Waitara aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ukonga pamoja na aliyekuwa Mbunge wa Monduli Julius Kalanga.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
