Mwanamuziki mkongwe nchini Tanzania, Ray C amedai kwamba asilimia kubwa ya watanzania hawajui kuitumia mitandao ya kijamii ipasavyo ili iwaingizie fedha, na badala yake wanaitumia kwa kujadili mambo yasiyo na tija kwa mtu mwenyewe na taifa kwa ujumla.
Ray C ameeleza hayo wakati akizungumza na www.eatv.tv hii leo Agosti 23, 2018, na kusema watu wengi wamekuwa wakipoteza muda na fedha zao kuingia kwenye mitandao hiyo bila ya kufikiria ni jinsi gani itaweza kuwarudishia faida.
"Watu wengi mitandaoni wanapenda upuuzi, ukiweka kitu cha maana hakuna mtu ambaye ata 'comment' chochote katika hicho ulichokiweka, maana wanakichukulia poa lakini fanye kinyume chake hapo ndio utawajua walipo. Wenzetu Ulaya mitandao ya kijamii kama wakina Kim Kardishian na wengine wanatumia mitandao hiyo kuuza 'product' na kuonyesha kazi zao ili wapate pesa...
lakini sisi ndio tumekuwa wakutoa pesa kwa kununua bando ili tukaharibu, tena sana sana Tanzania hatujui kutumia mitandao ili itunufaishe na badala yake tunatumia kwenye upuuzi", amesema Ray C.
Mbali na hilo, Ray C amedai hasumbuki na maneno ambayo amekuwa akizungumziwa kwenye mitandaoo ya kijamii kwa kuwa ana wafahamu watanzania vizuri jinsi walivyo.
"Huwezi kuzuia watu kuongea wanachokifikiria, Nikiingia kwenye mitandao ya kijamii siendi tu kukurupuka na kuweka kitu chochote bila ya kuwa na uhakika wa jambo fulani. Lakini wenye akili pungufu wanaweza wasinielewe ninachokizungumza ila wale wenye akili timamu watakuwa wananielewa", amesisitiza Ray C.
Kauli hizo za Ray C zimekuja baada ya siku za hivi karibuni kushambuliwa kwenye mitandao ya kijamii, baada ya yeye kuonekana kimbele mbele katika kila jambo licha ya kutokuwa muhusika katika hilo, na kufanya watu wadai pengine anatafuta kiki ili aweze kuendelea kuwa gumzo kwenye midomo yao.
Source
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Siku moja baada ya Israel kusema kuwa inazidisha uvamizi wake wa ardhini nchini Lebanon, Hezbollah inadai iliwafukuza wanajeshi wa Israel ...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...