Marekani imepiga marufuku uagizaji wa nguo kutoka Rwanda , baada ya taifa hilo la Afrika mashariki kupiga marufuku uingizaji wa mitumba na viatu nchini humo kutoka Marekani.
Rais Donald Trump ametoa agizo hilo akipiga marufuku uondoaji wa ushuru kwa nguo zote zinazotoka Rwanda kwa miezi sita baada ya kukutana na rais Paul Kagame na kumuita rafiki yake.
Kulingana na agizo hilo jipya ni wazi kwamba nguo za Rwanda hazitaingia tena katika soko la nchi hiyo bila kutozwa ushuru.
Ukweli wa mambo: Kwa nini baadhi ya nchi za Afrika hazitaki nguo za msaada
Serikali ya Marekani inasema kuwa Rwanda imeshindwa kuafikia masharti ya sheria ya AGOA iliopitishwa miaka 18 iliopita kuruhusu bidhaa zaidi za Afrika kuingia nchini Marekani.
Rwanda iliuza nguo zenye thamani ya dola milioni 1.5 nchini Marekani mwaka 2017 lakini hiyo ni asilimia 3 pekee ya bidha inazouza nchini Marekani.
Mwaka 2016, ,majirani wa Afrika mashariki Kenya, Tanzania na Rwanda zilikubaliana kupiga marufuku nguo zilizotumika pamoja na viatu kufikia 2019 ili kulinda viwanda vya nchini .
Kenya na Tanzania zilisalimu amri baada ya Marekani kutishia kupiga marufuku bidhaa zao zinazoelekea nchini humo lakini Rwanda imeendelea kuwekea ushuru mkubwa nguo hizo pamoja na viatu.
Rais Trump na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame walijadili biashara walipokutana mnamo mwezi Januari nchini Switzerland lakini hakuna hata mmoja wao aliyezungumzia mzozo kuhusu nguo hizo.
Marekani inadai kwamba marufuku dhidi ya nguo zilizotumika barani Afrika itawanyima raia 40,000 kazi , lakini Rwanda imesema kwamba haitakubali kuwa 'jaa'.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
