Marekani imepiga marufuku uagizaji wa nguo kutoka Rwanda , baada ya taifa hilo la Afrika mashariki kupiga marufuku uingizaji wa mitumba na viatu nchini humo kutoka Marekani.
Rais Donald Trump ametoa agizo hilo akipiga marufuku uondoaji wa ushuru kwa nguo zote zinazotoka Rwanda kwa miezi sita baada ya kukutana na rais Paul Kagame na kumuita rafiki yake.
Kulingana na agizo hilo jipya ni wazi kwamba nguo za Rwanda hazitaingia tena katika soko la nchi hiyo bila kutozwa ushuru.
Ukweli wa mambo: Kwa nini baadhi ya nchi za Afrika hazitaki nguo za msaada
Serikali ya Marekani inasema kuwa Rwanda imeshindwa kuafikia masharti ya sheria ya AGOA iliopitishwa miaka 18 iliopita kuruhusu bidhaa zaidi za Afrika kuingia nchini Marekani.
Rwanda iliuza nguo zenye thamani ya dola milioni 1.5 nchini Marekani mwaka 2017 lakini hiyo ni asilimia 3 pekee ya bidha inazouza nchini Marekani.
Mwaka 2016, ,majirani wa Afrika mashariki Kenya, Tanzania na Rwanda zilikubaliana kupiga marufuku nguo zilizotumika pamoja na viatu kufikia 2019 ili kulinda viwanda vya nchini .
Kenya na Tanzania zilisalimu amri baada ya Marekani kutishia kupiga marufuku bidhaa zao zinazoelekea nchini humo lakini Rwanda imeendelea kuwekea ushuru mkubwa nguo hizo pamoja na viatu.
Rais Trump na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame walijadili biashara walipokutana mnamo mwezi Januari nchini Switzerland lakini hakuna hata mmoja wao aliyezungumzia mzozo kuhusu nguo hizo.
Marekani inadai kwamba marufuku dhidi ya nguo zilizotumika barani Afrika itawanyima raia 40,000 kazi , lakini Rwanda imesema kwamba haitakubali kuwa 'jaa'.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Geneva, Switzerland /AFP /.More than 100 groups urged the International Labour Organization to stop taking money from tobacco companies as t...