Thursday, August 9, 2018

MAMIA WAJITOKEZA KUAGA MWILI WA MZEE MAJUTO DAR

Mamia ya waombolezaji wamejitokeza katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam kuaga mwili wa aliyekuwa muigizaji nguli wa vichekesho nchini, Amri Athumani 'Mzee Majuto' leo Agost 9, 2018.


Mzee King Majuto alifariki dunia jana majira ya saa 2:00 usiku Agosti 8, 2018 katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu kwa siku kadhaa.


Baada ya kuaga mwili utasafirishwa kwenda nyumbani kwake jijini Tanga kwa maziko ambayo yatafanyika kesho Ijumaa.

Tazama Video hapo chini




Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...