Kiongozi wa juu wa upinzani nchini Zimbabwe Tendai Biti amekamatwa Jumatano wiki hii katika mpaka wa Zambia wakati ambapo chama chake kinaendelea kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais, amebaini mwanasheria wake.
Tume ya Uchaguzi nchini Zimbabwe (ZEC) ilimtangaza Emmerson Mnangagwa, kuwa alishinda uchaguzi huo kwa asilimia 50.8.
"Amekamatwa kwenye mpaka wa Zambia," Nqobizitha Millo amesema, akiongeza kwenye ujumbe wa simu (SMS) kwamba waziri huyo wa zamani alikuwa akitafuta "hifadhi" ya ukimbizi katika nchi jirani ya Zambia.
Mmoja kati ya viongozi wa juu wa upinzani, na waziri wa zamani wa Fedha wa Serikali ya Umoja wa kitaifa (mnamo mwaka 2009-2013), Biti anatafutwa na mahakamani, wbaada ya kushtumiwa kuchochea vurugu, kwa mujibu wa gazeti la The Chronicle, linalounga mkono serikali.
Bw Biti alitangaza kabla ya kutangazwa rasmi matokeo ya uchaguzi na Tume ya Uchaguzi kwamba Nelson Chamisa, mgombea wa chama chake cha Movement for Democratic Change (MDC) alishinda uchaguzi, huku akiishtumu Tume ya Uchaguzi kwa kutangaza matokeo tofauti.
Tume ya uchaguzi ilimtangaza Bw Mnangagwa, aliyekuwa mshirika wa karibu wa Robert Mugabe, aliyetimuliwa madarakani na jeshi mnamo mwezi Novemba baada ya miaka 37 ya kuitawala nchi hiyo, mshindi wa uchaguzi huo kwa asilimia 50.8.
Hatua ya vikosi vya usalama na ulinzi kuvunja maandamano ya upinzani ilisababisha watu sita kupoteza maisha.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Mamlaka za China zipo mbioni kudhibiti ongezeko la harusi za kifahari amabazo zimekuwa zikishamiri katika miaka ya karibuni. Kwamujibu wa ma...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...