Tuesday, August 14, 2018
BREAKING: CCM yawarudisha tena Waitara, Kalanga kwa wananchi
Kamati Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) leo imekutana na kufanya kikao chake ambacho kimepitisha majina ya wagombea wa ubunge watatu katika majimbo matatu ya Ukonga, Korogwe Vijijini na Monduli.
Majimbo hayo yalitangazwa kuwa wazi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) baada ya mbunge wa Ukonga kujiondoa Chadema na kujiunga na CCM na mbunge wa Monduli naye kujiondoa Chadema na kujiunga na CCM na kwa upande wa Korogwe Vijijini mbunge wake alifariki dunia.
Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Dkt. John Magufuli ambaye aliongoza kikao hicho katika ofisi ndogo za CCM zilizoko Lumumba Jijini Dar es Salaam ametaja majina ya wagombea waliopitishwa kuwa ni Julius Kalanga Laizer jimbo la Monduli, Mwita Mikwabe Waitara jimbo la Ukonga na Timotheo Paul Mzava jimbo la Korogwe Vijijini.
Wakati huo huo Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt. John Magufuli amewashukuru na kuwapongeza Watanzania kwa kuipatia CCM ushindi wa asilimia 100 katika uchaguzi mdogo uliomalizika kwa kuiwezesha kutwaa jimbo la Buyungu Kigoma na kata zote 77.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
