Tuesday, August 14, 2018

BREAKING: CCM yawarudisha tena Waitara, Kalanga kwa wananchi


Kamati Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) leo imekutana na kufanya kikao chake ambacho kimepitisha majina ya wagombea wa ubunge watatu katika majimbo matatu ya Ukonga, Korogwe Vijijini na Monduli.

Majimbo hayo yalitangazwa kuwa wazi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) baada ya mbunge wa Ukonga kujiondoa Chadema na kujiunga na CCM na mbunge wa Monduli naye kujiondoa Chadema na kujiunga na CCM na kwa upande wa Korogwe Vijijini mbunge wake alifariki dunia.

Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Dkt. John Magufuli ambaye aliongoza kikao hicho katika ofisi ndogo za CCM zilizoko Lumumba Jijini Dar es Salaam ametaja majina ya wagombea waliopitishwa kuwa ni Julius Kalanga Laizer jimbo la Monduli, Mwita Mikwabe Waitara jimbo la Ukonga na Timotheo Paul Mzava jimbo la Korogwe Vijijini.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt. John Magufuli amewashukuru na kuwapongeza Watanzania kwa kuipatia CCM ushindi wa asilimia 100 katika uchaguzi mdogo uliomalizika kwa kuiwezesha kutwaa jimbo la Buyungu Kigoma na kata zote 77.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...