Tuesday, August 14, 2018
BREAKING: CCM yawarudisha tena Waitara, Kalanga kwa wananchi
Kamati Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) leo imekutana na kufanya kikao chake ambacho kimepitisha majina ya wagombea wa ubunge watatu katika majimbo matatu ya Ukonga, Korogwe Vijijini na Monduli.
Majimbo hayo yalitangazwa kuwa wazi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) baada ya mbunge wa Ukonga kujiondoa Chadema na kujiunga na CCM na mbunge wa Monduli naye kujiondoa Chadema na kujiunga na CCM na kwa upande wa Korogwe Vijijini mbunge wake alifariki dunia.
Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Dkt. John Magufuli ambaye aliongoza kikao hicho katika ofisi ndogo za CCM zilizoko Lumumba Jijini Dar es Salaam ametaja majina ya wagombea waliopitishwa kuwa ni Julius Kalanga Laizer jimbo la Monduli, Mwita Mikwabe Waitara jimbo la Ukonga na Timotheo Paul Mzava jimbo la Korogwe Vijijini.
Wakati huo huo Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt. John Magufuli amewashukuru na kuwapongeza Watanzania kwa kuipatia CCM ushindi wa asilimia 100 katika uchaguzi mdogo uliomalizika kwa kuiwezesha kutwaa jimbo la Buyungu Kigoma na kata zote 77.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Mamlaka za China zipo mbioni kudhibiti ongezeko la harusi za kifahari amabazo zimekuwa zikishamiri katika miaka ya karibuni. Kwamujibu wa ma...