Thursday, August 30, 2018

Bila Mimi Hakuna Ebitoke :-Mkali Wenu.

Msanii wa vichekesho Mkali wenu ambae  alipata umaarufu kwake kupitia mitandao ya kijamii amefunguka na kusema kuwa bila uwepo wake basi kusingekuwa na ebitoke anaefahamika katika tasnia ya sanii uapnde wa vichekesho. Ebitoke na Mkali wenu hawajajulikana kuna nini kati yao kwa sababu ebitoke aliwahi kumkana mwenzake hadharani ilhali wawili hao waliwahi kufanya kazi katikakundi moja hapo awali kabla hawajatengana . Hata hivyo Mkali Wenu anasema kuwa kama asingezaliwa na kuamua kuwa mwigizaj basi asingekuwepo ebitoke kama alivyo sasa hivi, ‘kama mimi nisingezaliwa na kuamua kuingi katika vichekesho basi hasingefahamika Ebitoke, Bwana mjeshi wala Mama ashura, kwa sababu hawa wamekuja baada ya mimi kuwa na clip zangu na kuzitambulisha katika kundi la timamu na ndipo wao walipotambulika kupitia kazi zangu hizo.’

The post Bila Mimi Hakuna Ebitoke :-Mkali Wenu. appeared first on Ghafla!Tanzania.


Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...