Saturday, March 22, 2025

Manara: Huu ni Mwaka wa Uchaguzi Msigombanishe Serikali na Wananchi Kwa Maswala ya Simba na Yanga




Serikali yaijia juu bodi ya ligi baada ya bodi ya ligi kutaka msaada kutoa serikalini na hii ni baada ya klabu ya yanga kudai alama tatu dhidi ya mpinzani wake simba lakini bodi ya ligi wameitupilia mbali hoja hiyo na hivyo imewataka wakae kikao na klabu ya yanga lakini klabu ya yanga awajataka kukaa kikao chochote kile na bodi ya ligi.

Aliyekua Msemaji wa Yanga amesema kuna uzushi unaendelea kuwa Serikali itaingia suala la Derby ya Kariakoo ambapo amesisitiza hata wao wameshabaini wenye mamlaka ya mpira wamekosea hivyo nao wamekaa pembeni hawataki kuchonganishwa na wananchi ikizingatiwa huu ni mwaka wa uchaguzi.

Kwamba Serikali haitaki kubeba mzigo wa mtu ,acha wahangaike nao wenyewe kwani serikali inajiandaa na msimu wa kampeni hivyo serikali haitaki kuingilia maswala kama hayo kwani ni jambo zito sana serikali kuingilia kati maswala ya kimchezo kwani sheria ya mpira aitaki serikali ijiusishe na maswala ya mpira kwani mpira utaongozwa na sheria na taratibu zake

Mpira wa Tanznia umekuwa na mpira wenye maendeleo makubwa sana hivyo basi chochote kinachofanyika ni kutia doa katika mpira huu kwani endapo serikali itaingilia kati maswala ya mpira litakuwa ni kosa kubwa na uenda ikasabisha ata Shirikisho la mpira duniani kuingilia kati

Bodi ya ligi wanatakiwa wajitathmini kwa hiki wanachokifanya kwani siyo kujenga mpira bali ni kubomoa na chanzo ya hayo yote ni baada y raisi wa mpira wa miguu Tanzania wallace karia kuongea maneno ambayo yalileta mijadala mingi sana mtandaoni kwani aikuwa sahihi kwa mtu kama yeye kuzungumza maneno kama yale siyo jambo zuri na alikustahili kuzungumzwa.


KLABU YA COASTAL UNION YAPOKEA BASI JIPYA KUTOKA BENKI YA NBC

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu wa Ligi Kuu ya NBC imekabidhi basi jipya kwa Klabu ya soka ya Coastal Union FC ya jijini Tanga inayoshiriki ligi hiyo ikiwa ni mwendelezo wa dhamira ya dhati ya benki hiyo katika kuboresha ligi hiyo.

Coastal Union FC inakuwa klabu ya nne inayoshiriki ligi hiyo kunufaika na mpango huo unaohusisha mkopo nafuu kutoka benki ya NBC baada ya klabu za KMC ya Kinondoni, Singida Big Stars na Namungo FC kunufaika na mpango kama huo hapo awali. Mkopo wa basi la Coastal Union FC unaifanya benki ya NBC kuwa imetoa jumla ya mikopo yenye thamani ya sh bil 1.2 kwenye usafiri wa vilabu hivyo vinne vilivyonufaika na mpango huo.

Hafla ya makabidhiano ya basi hilo iliyohusisha paredi maalum la basi hilo katika maeneo mbalimbali ya jiji la Tanga, imefanyika leo kwenye tawi la benki ya NBC jijini Tanga ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Bw. Zephania Stephan Sumaye aliemuwakilisha Mkuu wa Mkoa huo Balozi Dkt Batilda Burian.

Pia hafla hiyo ilihusisha uwepo wa Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga, Al-Hajj Abdulrahman Shiloow, viongozi waaandamizi wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya NBC, Elvis Ndunguru, Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union FC, Bw Muhsin Ramadhan Hassan, mdhamini wa klabu hiyo kampuni ya RATCO Express, benchi la ufundi pamoja na wachezaji.

Akizungumza kwa niaba ya Balozi Dkt Burian, DC Sumaye pamoja na kuipongeza benki hiyo kwa hatua hiyo muhimu, alisema hatua hiyo imekuja kipindi ambacho uongozi wa mkoa huo upo kwenye utekelezaji wa wito wa Rais Samia wa kuchochea kasi ya maendeleo mkoani humo ikiwemo sekta ya michezo kupitia uboreshaji wa miundombinu ya michezo.

"Kilichofanywa na NBC leo ni kama kuunga mkono muitikio wa wito huu wa Rais Samia. Nimevutiwa zaidi kuona NBC wanagusa hadi masuala ya bima kwa wanamichezo hilo ni jambo zuri zaidi. Ombi Langu kwa wachezaji na viongozi wa klabu ni kuhakikisha kwamba jitihada hizi zinatoa majibu kwenye matokeo ya uwanjani,'' alisema.

Awali akizungumza kwenye hafla hiyo iliyoambatana na msafara maalum kutoka kwenye tawi la NBC hadi Makao makuu ya klabu hiyo, Ndunguru alisema basi hilo ni sehemu ya mpango wa utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa vilabu vinavyoshiriki ligi hiyo.

"Ukosefu wa vyombo vya usafiri maalum kwa ajili ya timu zinazoshiriki ligi Kuu ya NBC imekua ni moja ya chanzo cha vikwazo vingi katika gharama za uendeshaji na utendaji wa timu husika.Jitihada zetu kama wadhamini haziishii hapa tu kwenye mikopo ya usafiri bali tunagusa maboresho ya baadhi ya viwanja vinavyotumia kwenye ligi hii, tunatoa bima za afya kwa wachezaji na mabenchi ya ufundi na zaidi tunatoa huduma za kifedha ikiwemo elimu ya kifedha kwa wadau wa michezo wakiwemo wachezaji,'' alisema.

Wakizungumza kwenye hafla hiyo Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union FC Bw Muhsin Ramadhan Hassan na Mstahiki Meya Al-Hajj Shiloow pamoja kuishukuru benki hiyo kwa jitihada zake za kuiboresha ligi hiyo walikiri kuwa klabu hiyo ilikuwa ikikabiliwa na changamoto ya usafiri bora hapo awali hali ambayo iliongeza changamoto katika ubora wat imu hiyo.

"Tanga sasa tumeweka alama kupitia benki ya NBC. Kupitia usafiri huu sasa tuna uhakika wa kusafirisha wachezaji wetu kwenda popote, wakati wowote tena wakiwa na utulivu zaidi.Ni wazi sasa tunakwenda kuongeza ushindani zaidi kwenye ligi kupitia hatua hii ya leo,'' alisema Mwenyekiti Muhsin.
Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Bw. Zephania Stephan Sumaye (wa pili kulia) akikabidhi mfano wa ufunguo kwa Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union FC ya jijini Tanga Bw Muhsin Ramadhan Hassan (wa pili kushoto) ikiwa ni ishara ya kumkabidhi basi lilotolewa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambaye ni Mdhamini Mkuu wa Ligi Kuu ya NBC.
Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya NBC, Elvis Ndunguru (katikati) akizungumza na viongozi, wanachama na mashabiki wa Klabu ya Coastal Union FC ya jijini Tanga alipotembelea makao makuu ya klabu hiyo jijini humo wakati wa hafla ya makabidhiano ya basi lililotolewa na benki ya NBC kwa klabu hiyo kama mkopo.
Baadhi ya wakazi wa jiji la Tanga wakifuatilia hafla fupi ya makabidhiano ya basi lililotolewa na benki ya NBC kama mkopo kwenda Klabu ya Coastal Union FC ya jijini Tanga. Hafla hiyo imefanyika leo kwenye tawi la NBC jijini Tanga.
Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Bw. Zephania Stephan Sumaye akizungumza na wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Mkuu wa Mahusiano ya Idara ya Mahusiano ya Umma na Mawasiliano wa NBC, Godwin Semunyu akizungumza na wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga, Al-Hajj Abdulrahman Shiloow akizungumza na wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union FC Bw Muhsin Ramadhan Hassan akizungumza na wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Meneja wa NBC Tawi la Tanga Bw Japhary Hassan akizungumza na wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Baadhi ya wachezaji wa Klabu ya Coastal Union FC wakiwa kwenye hafla hiyo.

Maajabu! MTI ULIOANGUSHWA NA UPEPO, UKAKATWA ,WASIMAMA TENA GEITA

 

Zaidi ya wakazi 1,000 wa Mtaa wa Mpomvu, Kata ya Mtakuja, katika Manispaa ya Geita wamekusanyika kushuhudia tukio la kushangaza baada ya mti ulioangushwa na upepo mkali uliombatana na mvua kubwa, ukakatwa, kusimama tena asubuhi iliyofuata.

 Tukio hilo limezua gumzo kubwa na hisia tofauti miongoni mwa wakazi wa eneo hilo.

Mti huo, unaomilikiwa na Kanisa la Golan Gospel Center lililopo mtaani hapo, umeibua mijadala kuhusu uwezekano wa tukio hilo kuwa la miujiza.

 Baadhi ya viongozi wa kanisa na wananchi wameeleza kushangazwa na hali hiyo.

Katibu wa Kanisa la GGC, Yohana Mathias, amesema tukio hilo limewashangaza waumini wa kanisa na wakazi wa Mpomvu, huku wengine wakilihusisha na nguvu za kiimani.

Mkazi wa Mpomvu, Emmanuel Lameck, amesema hajawahi kushuhudia jambo kama hilo maishani mwake na kwamba bado linafikirisha.

Naye Stella Saimon, mkazi wa Mpomvu, amekiri kuwa tukio hilo limeleta mshtuko kwa wengi, huku wengine wakitafsiri kuwa ni tukio la kiimani au la kishirikina.

Mchungaji wa Kanisa la Golan Gospel Center, Jefta Lameck, amesema mti huo ulikuwa wa muda mrefu, na baada ya kuangushwa na upepo, waliamua kuukata kwa kuwa ulikuwa umezuia njia. Hata hivyo, walipofika asubuhi iliyofuata, walikuta mti huo umesimama tena hali iliyozua mshangao mkubwa.

Amesema tukio hilo lisihusishwe na imani za kishirikina na amewataka wananchi kuwa watulivu huku wakilitafakari kwa mtazamo wa kawaida wa kimaumbile badala ya kuingiza hofu au imani potofu.


Chanzo - Maduka Online Blog

Wamarekani Hawautaki Ushirikiano wa TRUMP na Elon Mask, Washambulia Magari ya Tesla

 

Wamarekani Hawautaki Ushirikiano wa TRUMP na Elon Mask, Washambulia Magari ya Tesla

Mashambulizi dhidi ya vituo vya Tesla yameongezeka baada ya #ElonMusk kushirikiana na utawala wa #Trump kwenye Idara ya Ufanisi wa Serikali (#DOGE), ambayo imepunguza matumizi makubwa ya serikali.


Miji kama Portland na Seattle imeathirika zaidi, huku magari ya Tesla, vituo vya kuchaji, na stoo za magari vikilengwa. Kwenye shambulio moja #LasVegas, magari kadhaa yaliwashwa moto na neno "#resist" likaandikwa kwenye jengo.


Mwanasheria Mkuu wa Marekani, Pam Bondi, alisema watu watatu waliokamatwa kwa mashambulizi hayo wanakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 20 kwa ugaidi wa ndani.


Trump alitumia #TruthSocial kutangaza kuwa wahusika wanapaswa kufungwa kwa miaka 20 na kupendekeza wafungwe katika magereza ya #ElSalvador, akiyataja mashambulizi hayo kama ugaidi wa ndani. Alisisitiza kuwa Tesla ni "kampuni kubwa ya Marekani" na hata kununua gari lake la #Tesla kuonyesha uungaji mkono.

Friday, March 21, 2025

DR. MPANGO AWAFARIJI WAFIWA MSIBA WA HAWASSI



Na Mwandishi wetu,Dodoma

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango na Mwenza wake Mama Mbonimpaye Mpango wameshiriki msiba wa Bi. Damaris Hawassi ambaye ni Mke wa Katibu wa NEC (Uchumi na Fedha) wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Frank Hawassi katika makazi ya familia hiyo mtaa wa Miyuji Jijini Dodoma.

Akiwafariji waombolezaji katika msiba huo, Makamu wa Rais ametoa salamu za rambirambi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ametoa salamu za pole kwa familia na waombolezaji wote kufuatia msiba huo.

Makamu wa Rais amewaombea faraja wanafamilia pamoja na wote walioguswa na msiba huo. Amewashukuru wananchi waliojitokeza kuifariji familia katika kipindi hiki kigumu kwao.

Makamu wa Rais amesema ni vema Watanzania kuendelea kushirikiana katika changamoto mbalimbali zinapotokea katika jamii ikiwemo magonjwa na vifo kwa kudumisha undugu, amani na kupendana ili kuwa na Taifa zuri na lenye ustawi.

Halikadhalika Makamu wa Rais amesema Bi.Damaris Hawassi alikua mchapakazi hodari aliyetimiza vema wajibu wake katika umri aliyojaaliwa duniani. Ameongeza kwamba ni vema kujifunza juu ya kila mmoja kutimiza wajibu wake pamoja na kuishi vema na wanadamu wengine.





Ripoti Ya Ufuatiliaji wa Uwajibikaji wa Jamii Katika Malezi na Makuzi ya Awali ya Mtoto Yaonesha Changamoto Kadhaa Babati

Na John Walter -Babati 

Marafiki wa Elimu wilaya ya Babati wamewasilisha ripoti ya ufuatiliaji wa uwajibikaji wa jamii katika malezi na makuzi ya awali ya mtoto.

Ripoti hiyo, iliyowasilishwa na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Mji wa Babati, Benjamin Richard, inaonesha changamoto mbalimbali zinazowakabili watoto katika malezi, usalama, na mazingira ya kujifunzia.

Utafiti huu ulifanyika katika kata nne za Babati ,Bagara, Maisaka na Nangara kwenye shule za Msingi 16, ambapo wadau mbalimbali walihojiwa, wakiwemo watendaji wa kata, wamiliki wa vituo vya kulelea watoto (day care), walimu, wawakilishi wa asasi za kiraia, viongozi wa serikali za mitaa na vijiji, pamoja na wazazi wenye watoto katika shule za awali.

Matokeo Muhimu ya Ripoti

  1. Usalama wa Watoto Shuleni

    • Kati ya shule 16 zilizotembelewa, hakuna hata moja yenye uzio, hali inayohatarisha usalama wa watoto.
    • Shule nyingi zipo karibu na barabara, hivyo kuongeza hatari kwa watoto.
  2. Adhabu kwa Watoto

    • Asilimia 11.2 ya waliohojiwa walithibitisha kuwepo kwa adhabu za kuumiza katika baadhi ya shule.
    • Hata hivyo, asilimia 60 ya wazazi na walimu walikiri kuwa shule ni salama na wanatambua umuhimu wa ulinzi na usalama wa watoto.
  3. Afya na Mazingira ya Shule

    • Asilimia 68 ya vyoo vya shule si salama kwa watoto, hali inayohatarisha afya zao.
    • Ni shule tano pekee ndizo zenye vyoo maalum kwa wanafunzi wa awali.
  4. Malezi na Muda wa Wazazi na Watoto

    • Asilimia 93.7 ya watu 168 waliohojiwa walikiri kuwa wazazi wengi hawana muda wa kukaa au kucheza na watoto wao.
    • Wazazi wengi wamekuwa wakiacha majukumu yao kwa wafanyakazi wa ndani, ambao mara nyingi huonekana kama mama na baba wa watoto hao.

Hatua Zinazochukuliwa

Baada ya uwasilishaji wa ripoti hii, Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha Marafiki wa Elimu Babati, Gaudencia Igoshalimo, amesema kuwa watarejea kwa wananchi kwa ajili ya kuhamasisha marekebisho ya changamoto zilizobainika.

Marafiki wa Elimu Babati, chini ya mwavuli wa HakiElimu, wanatekeleza miradi mbalimbali ya kuboresha mazingira ya watoto, ikiwa ni pamoja na:

  • Ujenzi wa vyoo katika shule tano ili kuboresha usafi na usalama wa wanafunzi.
  • Ujenzi wa bweni katika Shule ya Sekondari Nakwa, ambapo wazazi watachangia ujenzi wa msingi na HakiElimu itakamilisha mradi huo.

Wito kwa Wazazi

Wazazi wametakiwa kutenga muda wa kukaa na watoto wao badala ya kuwaachia malezi kwa wafanyakazi wa ndani pekee.

 "Wazazi waache tabia ya kuwa bize na maisha huku wakitelekeza watoto wao, ni jukumu la mzazi kuhakikisha mtoto anapata malezi bora na muda wa kufundwa katika misingi sahihi ya maisha," ilisisitizwa katika ripoti hiyo.

Kwa hatua hii, Marafiki wa Elimu Babati wanaendelea kushirikiana na jamii kuhakikisha kuwa watoto wanalelewa katika mazingira salama, yenye afya, na yanayochochea maendeleo yao ya elimu na maisha kwa ujumla.

Picha mbalimbali wakati wa Uwasilishaji ripoti.








Bosi Hakujua Kama Nimemfunga Mke wangu

Bosi Hakujua Kama Nimemfunga Mke wangu


Jina langu Abdallah, unajua wahenga hawakukosea waliposema ukistaajabu ya musa utayaoana ya firauni, huu ni msemo ambao hadi sasa unaishi katika maisha ya watu na jamii kwa ujumla kutokana na matukio na visa mbalimbali vinavyowakumba.

Singependa kutaja jina langu kutokana sababu za kiusalama ila naishi nchini Kenya, nimeamua kuandika ujumbe huu baada ya Bosi wangu kuleta mambo ya ajabu sana, nayo ni kung'ang'ania kuzaa mtoto na mke wangu wa ndoa.

Hata hivyo, mke wangu hakujua kama nimemfunga, wala Bosi wangu hakujua hilo, hivyo nilipokuwa napata safari za kikazi nilikuwa na amani tele na furaha zaidi hasa kutokana na kuongezeka kwa fedha ambayo nilikuwa napatiwa kama posho ya kujikimu na safari.

Baada ya muda wa miezi kadhaa mke wangu aliniita chumbani na kuniambia Bosi wangu alikuwa akimtongoza na kumwambia anataka kuzaa naye kutokana anaona watoto wetu ni wazuri sana na wanavutia.

Mke wangu aliniambia kwa muda mrefu alifanya jambo hilo kuwa siri lakini anaona kadiri anavyofanya siri moyo wake unakosa amani kabisa kutokana na jinsi anavyosumbuliwa.

Alilia sana na kuniomba msamaha kwa kutunza siri hiyo ya ajabu ambayo ingeweza kumfanya akazaa nje ya ndoa yetu ambayo imedumu kwa miaka mingi sasa, huku ikiwa na amani na upendo.

Hadi kufika hapo nikajua kabisa dawa ya Kiwanga Doctors kweli inafanya kazi yake ipasavyo, kilichokuja kunishangaza ni yule Bosi wangu alikuja kufukuzwa kazi katika mazingira ambayo sikuwahi kuyaelewa hadi sasa na hapo ndoa yangu ikazidi kuwa na usalama zaidi.

Unajua tulifikaje hapo?. kwa uwezo wa Kiwanga Doctors kutoka Migori, Kenya ndipo nilipobaini mbinu hiyo chafu ya Bosi wangu, nakumbuka nafiki yangu mmoja alinipa namba ya mtaalamu huyo na kuniambia anaweza kumfunga mke wangu asiweze kutoka nje ya ndoa.

Nilifika ofisini kwake na alinipatia dawa na kuanza kuzitumia, niliendelea na shughuli zangu, wakati huo Bosi wangu alikuwa kila mara ananipa safari nyingi za kikazi ili apate muda wa kuendelea kumshawishi mke wangu bila kujua tayari nilishamfunga.

Kwa hakika ni watu wengi wamepata uponyaji, mafanikio, furaha kupitia huduma za Kiwanga Doctors ambao unaweza kuwasiliana na kwa namba +254 116469840 au tembelea tovuti yao, www.kiwangadoctors.co.tz kwa maelezo zaidi kuhusu huduma zao.

Ommy Dimpoz Amefukuzwa na GSM na kuachishwa Kazi? Aandika haya baada ya tetesi kusambaa

 Ommy Dimpoz amefukuzwa na GSM na kuachishwa kazi? Aandika haya baada ya tetesi kusambaa


Thursday, March 20, 2025

JUHIBU Yaja na Mbinu Mpya Kukabiliana na Wanyamapori Waharibifu

Na John Walter -Babati

Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Burunge (JUHIBU) imeendelea kubuni mbinu mbalimbali za kuzuia wanyamapori waharibifu kuvamia mashamba na kula mazao ya wakulima.

Katika juhudi hizo, JUHIBU imeanzisha matumizi ya baruti, pilipili na mchanga vilivyowekwa kwenye mipira ya kondomu kama moja ya njia za kuwazuia wanyama hao kuingia kwenye mashamba ya wananchi.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Kaganda, amekabidhi vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni 76 vya kuimarisha ulinzi wa mashamba kwa vijiji 10 vya kata ya Mwada, Nkaiti na Magara vinavyohudumiwa na JUHIBU.

Kwa mujibu wa Katibu wa JUHIBU Benson Mwaise, Vifaa hivyo ni pamoja na vilipuzi na honi, ambavyo vinalenga kusaidia wakulima kuwatisha wanyama waharibifu na hivyo kuwaepusha na hasara ya mazao yao.

Amesema kuwa hatua hiyo inalenga kupunguza migogoro kati ya binadamu na wanyamapori, hasa katika maeneo yanayopakana na hifadhi za wanyama.

"Tunapenda kuona wakulima wakiendelea kufanya shughuli zao bila hofu ya wanyama waharibifu, huku tukihakikisha kuwa wanyama hawa wanahifadhiwa kwa njia endelevu," alisema Kaganda.

JUHIBU imekuwa mstari wa mbele katika kutafuta suluhisho endelevu kwa changamoto hiyo, kwa kushirikiana na serikali na wananchi kuhakikisha wanyama na binadamu wanaishi kwa amani bila kuathiri ustawi wa pande zote mbili.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...