Tanzania Daily Eye
Sunday, October 12, 2025
Serikali yazindua mfumo wa kielektoniki ukaguzi wa vyombo vya Moto.
Friday, October 10, 2025
Mgombea wa CCM Mabibo atangaza neema rukuki
MGOMBEA Udiwani wa Kata ya Mabibo, wilayani Ubungo, jijini Dar es Salaam, kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ashura Mohammed Seg'ondo, amewataka wananchi katika kata hiyo kujitokeza kwa wingi Oktoba 29 mwaka huu kumpigia kura Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan na yeye kwa nafasi ya udiwani ili kuwaletea maendeleo ya haraka.
Aidha amewataka kumchagua Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM katikaJimbo la Ubungo Profesa Kitila Mkumbo hali itakayo harakisha maendeleo katika kata hiyo.
Akihutubia mkutano wa kampeni katika kata hiyo, Ashura alisema akichaguliwa kipaumbele chake cha kwanza ni kuhakikisha anasimamia kikamilifu ujenzi wa miundo mbinu.
"Miundombinu nimeigawanya katika sehemu mbili. Barabara kuu na barabara za ndani. Katika Mtaa wa Jitegemee mkandarasi tayari anaendelea na ujenzi wa Barabara ya Binti Kayenga. Nami kwa kushirikiana na nyie nitahakikisha kwa ujasiri wangu mkubwa kwa nguvu zangu zote mkandarasi afanye kazi kwa haraka kukamilisha ujenzi,"ameeleza Ashura.
Amebainisha, Kata ya Mabibo, imejaaliwa viwanda vikubwa hivyo kwa kushirikiana na viongozi atahakikisha kwa asilimia kubwa wakazi wa kata hiyo watananufaika na ajira.
"Pia katika sekta ya michezo nitahakikisha tunashirikiana vyema ili iwe fursa ya ajira kwa sababu Kata ya Mabibo ni ni kitovu cha mchezo wa ngumi. Bondia Mfaume Mfaume anatoka katika kata hiii,"ameeleza.
Kuhusu mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri , Ashura ameeleza atahakikisha inawasikia walengwa.
"Mikopo inakuja lakini haiwanufaishi walengwa. Nikichaguliwa nitahakikisha mikopo hii inawafikia walengwa. Inawanufaisha wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Kausha damu itakuwa baibai,"ameeleza mgombea huyo.
Amesema atafanya jitihada kuleta walimu wa vikoba kutoa elimu kwa wananchi katika kata hiyo ili viinue uchumi hasa wawanawake.
Friday, October 3, 2025
TAMASHA LA SIKU YA WANA 'STAND UNITED" NI KESHO JUMAMOSI CCM KAMBARAGE
Tuesday, September 30, 2025
RAIS SAMIA ALETA MWANGA WA ELIMU KWENYE VIJIJI KAHAMA




Source
CMSA Yaipongeza Tanga Saruji kuzindua Mauzo ya Hisa Stahiki za Bilioni 204
Kampuni ya Tanga Saruji imeweka historia mpya katika masoko ya mitaji nchini Tanzania kwa kuzindua rasmi mauzo ya Hisa Stahiki zenye thamani ya jumla ya shilingi bilioni 204. Hii ni mara ya kwanza kwa kampuni nchini kutoa hisa stahiki za thamani kubwa kuwahi kushuhudiwa katika historia ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), hatua inayotajwa kuwa ya kimkakati katika kuimarisha uwekezaji na kuongeza thamani kwa wanahisa.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), CPA Nicodemus Mkama aliipongeza Bodi na Menejimenti ya Kampuni ya Saruji Tanga kwa uongozi thabiti, ujasiri na maono ya kimkakati yaliyopelekea mageuzi makubwa ya kiutendaji ndani ya kampuni hiyo.
"CMSA tunaridhishwa na hatua za mabadiliko ya kimkakati yanayoendelea katika kampuni hii, ikiwa ni pamoja na kupunguza mikopo ya kigeni, kuongeza mapato na faida ya kampuni, na kutoa fursa zaidi za uwekezaji kwa wananchi," alisema CPA Mkama
Hisa hizi stahiki zinauzwa kwa wanahisa wa sasa wa Kampuni ya Tanga Saruji kwa bei ya shilingi 1,600 kwa hisa moja, ambayo ni punguzo la asilimia 38.2 ukilinganisha na bei ya soko ya shilingi 2,590 kwa hisa moja. Kiasi cha hisa kinachotolewa ni 127,342,090, katika uwiano wa hisa mbili kwa kila hisa moja anayomiliki mwekezaji kwa sasa.
Aidha Utoaji huo wa hisa umetajwa kuwa umekidhi kikamilifu matakwa ya Sheria ya Masoko ya Mitaji na Dhamana, Sura ya 79 ya Sheria za Tanzania pamoja na Kanuni zake, baada ya kupokea idhini rasmi kutoka CMSA.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi, ongezeko la thamani ya hisa za Kampuni ya Saruji Tanga limekuwa kubwa kwa kipindi cha muda mrefu – kutoka shilingi 300 mwaka 2002 hadi shilingi 2,590 kwa hisa moja mwaka 2025, sawa na ongezeko la asilimia 763.3.
"Tunaipongeza Kampuni ya Tanga Saruji kwa mafanikio haya makubwa. Hili ni somo na mfano kwa kampuni nyingine zilizo orodheshwa katika soko la hisa kuendelea kuboresha ufanisi na utawala bora," aliongeza CPA Mkama.
Aidha, alieleza kuwa mafanikio ya Tanga Cement ni uthibitisho wa nafasi muhimu ya masoko ya mitaji katika kukuza uchumi wa Taifa, kwa kutoa mitaji ya muda mrefu kwa kampuni, kusaidia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhamasisha umiliki wa pamoja wa rasilimali za uzalishaji.
Pia CPA Mkama amesisitiza kuwa mafanikio hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 (TDV 2050), ambayo inalenga kuifikisha Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati wa juu na kufikia Pato la Taifa la Dola Trilioni 1 ifikapo mwaka 2050.
Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) pia imepongeza wadau waliohusika katika mchakato wa maandalizi ya Waraka wa Matarajio, akiwemo mshauri kiongozi wa kifedha iTrust Finance Limited, Mshauri wa Kisheria Joachim & Jacobs Attorneys, pamoja na wakaguzi Deloitte & Touche, kwa weledi wao mkubwa uliofanikisha hatua hii muhimu.
Mchakato wa mauzo ya hisa hizo unatarajiwa kufungwa Oktoba 24, 2025, na wanahisa wametakiwa kuchangamkia fursa hiyo adhimu ya kuongeza uwekezaji wao kwa bei ya punguzo.
"Napenda kutoa wito kwa wanahisa wote kutumia fursa hii kununua hisa stahiki, ili kuimarisha uwekezaji wao na kuwa sehemu ya mafanikio endelevu ya kampuni hii ya kihistoria," aliongeza
CPA Mkama pia amezitaka kampuni nyingine katika sekta binafsi na umma kutumia kikamilifu masoko ya mitaji kama chanzo mbadala cha fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, badala ya kutegemea mikopo ya gharama kubwa.
Friday, September 19, 2025
MWANA FA KUSHUGHULIKIA MAWASILIANO YA SIMU JIMBO LA MUHEZA

Na Mwandishi Wetu, Muheza
MGOMBEA ubunge Jimbo la Muheza kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Hamis Mwinjuma maarufu MwanaFA amesema katika miaka mitano ijayo atahakikisha anaongeza minara ya simu ili Jimbo la Muheza liweze kuwa na mawasiliano katika maeneo ambayo yana changamoto hiyo.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika kata ya Kwezitu tarafa ya Amani, MwanaFA alikiri kwamba yapo maeneo katika Jimbo hilo, yana changamoto ya ukosefu wa mawasiliano.

"Katika miaka mitano ijayo tutaimarisha mawasiliano ya simu...Moja ya mambo yanayonisikitisha ni kufika baadhi ya maeneo kwenye Jimbo la Muheza ikawa simu haiwezi kushika mawasiliano, huwezi kupigiwa simu," alisema na kuongeza,
"Tunachotaka kufanya ni kuhakikisha tunaongeza minara ya simu ili kuongeza kiwango cha upatikanaji wa mawasiliano kwa wananchi wetu,".

MwanaFA ambaye ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, alisema kuwa katika kipindi cha mwaka 2020-2025 Jimbo hilo lilipata minara Saba ambayo kutokana na jiografia ya Jimbo hilo, bado haijakidhi mahitaji ya mawasiliano katika maeneo mengi kutokana na hali hiyo.
Hivyo, alisema anakwenda kuzifanyia kazi kuhakikisha minara ya simu inaongezeka na hali ya mawasiliano inazidi kuimarika katika Jimbo hilo.

"Sitaki kuahidi mambo mengi na nikashindwa kuyatekeleza lakini niwahakikishie jambo moja changamoto zote za kata ya Kwezitu, Jimbo la Muheza kwangu ni kipaumbele...Miaka mitano hii nimejua kona zote za kutatua changamoto zilizopo katika Jimbo letu," alisema.
Aliwaomba wananchi wa Kwezitu kufanya kazi mbili ambazo ni kwenda kupiga kura Oktoba 29 na kuwachagua wagombea wa CCM ili waweze kumalizia kazi ambazo wamezifanya katika miaka mitano iliyopita.

Alisema wananchi wa Kwezitu wanakila sababu za kumchagua Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwakuwa ameleta fedha nyingi katika kata hiyo na Jimbo zima la Muheza.
Rais ameleta fedha nyingi katika miradi ya afya, elimu, maji, barabara na miradi mingine hivyo anastahili kupigiwa kura nyingi katika Jimbo letu.
"Nichagueni na Mimi miaka mitano hii nimeisema wilaya hii, hatuwezi kusema matatizo yetu yote tumeyamaliza bali dhamira yetu ni ya dhati kwakuwa kila sekta tumeigusa," alisema na kuwaomba wananchi wa kata hiyo kumchagua Mch. John Mzalia awe diwani wa kata hiyo.

Akiomba kura kwa wananchi wa kata hiyo Mgombea udiwani Mch Mzalia alisema kuwa kata hiyo imepata miradi mingi kuliko wakati wowote ule ikiwemo miradi ya Elimu, afya, barabara na huduma za jamii.
"Tumepata mradi wa Boost ambao shule yetu ya Kwezitu imekuwa nzuri mno hadi watoto wetu wanasoma kwenye shule ya vioo wakati mwingine wanachungulia kwenye madirisha hayo kama watoto wa Kihindi," alisema na kuwaomba wananchi hao wawachague wagombea wa CCM.
Katibu wa CCM wilaya ya Muheza Simon Leng'ese amewataka viongozi wa CCM wa ngazi zote za kata hiyo kuhakikisha wanatoka na kwenda kwa wananchi kuomba kura za wagombea wa CCM ili kukifanya chama hicho wagombea wake kupata kura za kishindo.

"Viongozi wa kata, matawi, mashina, mabalozi mtoke kwenda kuomba kura kwa wananchi katika maeneo yenu, haya ni maagizo nawapa mwende kukifanya chama chetu na wagombea wetu waweze kupata kura nyingi," alisema Leng'ese.
Meneja wa kampeni wa mgombea wa Jimbo la Muheza Aziza Mshakang'oto ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM wilaya ya Muheza (UVCCM), amewataka wananchi wa kata ya Kwezitu wasifanye makosa kwa kuwachagua wagombea wa upinzani kwakuwa hawana jipya.
Alisema CCM imekuja na ilani ambayo kwa wilaya ya Muheza imekuwa na miradi mingi ya maendeleo katika Jimbo hilo hivyo wasifanye makosa katika uchaguzi huo.
Mwisho
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...