
Tanzania Daily Eye
Wednesday, July 2, 2025
JUMBE AREJESHA FOMU YA UBUNGE SHINYANGA MJINI... "ZOEZI LIMEENDA VIZURI, CCM IMEWEKA MAZINGIRA BORA KWA WATIA NIA"

FAHAD AJITOSA UBUNGE SHINYANGA MJINI KUPITIA CCM: AVUNJA UKIMYA TETESI ZA ACT-WAZALENDO


Tuesday, July 1, 2025
Naibu waziri Sillo awajulia hali majeruhi ajali ya Same.
Wednesday, June 25, 2025
RAIS SAMIA AMEWEKA ALAMA KWA WATUMISHI WA MAGEREZA ARUSHA, AWAGAWIA MITUNGI 528

Source
Wakulima Babati Wavutwa Kulima Karanga Baada ya Utafiti wa TARI
TRA SHINYANGA YATOA ELIMU YA KODI KWA WANACHUO CHA UFUNDI STADI VETA

Semina hiyo imefanyika leo Juni 25, 2025 katika Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Shinyanga kilichopo manispaa ya Shinyanga.
Akizungumza wakati wa semina hiyo, Afisa wa kodi kutoka TRA Shinyanga Semeni Mbeshi, amesema lengo ni kuwajengea msingi mzuri wa kizalendo vijana wanaotarajia kuingia kwenye soko la ajira na kujiajiri baada ya kuhitimu masomo yao.
Ameongeza kuwa elimu hiyo ni endelevu na inalenga kujenga taifa la watu waaminifu katika ulipaji wa kodi, huku akisisitiza matumizi ya IFD kwa wafanyabiashara na kutoa na kudai risiti pindi wanaponunua bidhaa.
"Haki ya mlipa kodi ni kuaminiwa pindi anapofika kwenye ofisi za TRA kwa ajili ya kufanyiwa makadilio yanayoendana na biashara yake, ni wajibu wa kila mfanyabiashara kutoa taarifa ya ufanyaji wa biashara kwa mamlaka ya mapato TRA, utoaji wa risiti za IFD zinasaidia kuweka rekodi sahihi ya kumbukumbu ya biashara kwa muda wa miaka 5, lakini kodi hiyo inakwenda moja kwa moja kwenye mfuko wa serikali na kuwezesha maendeleo kwenye taifa letu", amesema Semeni Mbeshi.
Kwa upande wake, Mkufunzi katika Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Shinyanga, Emili Shirima amesema vitendo vya baadhi ya watu kutumia vishoka kujipatia huduma za kikodi si sahihi na ni hatari kwa uchumi wa taifa, alisema na kuwataka wanachuo kujiepusha na tabia hizo mara watakapoingia kwenye shughuli za uzalishaji mali.
Baadhi ya wanachuo walioshiriki mafunzo hayo wameishukuru TRA kwa kuwapa elimu hiyo muhimu, wakisema itawasaidia mara baada ya kuhitimu na kuanzisha biashara au shughuli za kujitegemea na kuo ngeza kuwa sasa anaelewa kwamba ulipaji wa kodi unasaidia huduma za jamii kama afya, elimu na miundombinu.
Afisa wa kodi kutoka TRA Shinyanga Semeni Mbeshi akizungumza wakati wa mafunzo hayo.



















Tuesday, June 24, 2025
SERIKALI YAZIDI KUHAMASISHA NISHATI SAFI, YATOA MITUNGI 225 KWA WATUMISHI GEREZA KUU MAWENI











-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...