Tanzania Daily Eye
Saturday, March 22, 2025
Manara: Huu ni Mwaka wa Uchaguzi Msigombanishe Serikali na Wananchi Kwa Maswala ya Simba na Yanga
KLABU YA COASTAL UNION YAPOKEA BASI JIPYA KUTOKA BENKI YA NBC
Maajabu! MTI ULIOANGUSHWA NA UPEPO, UKAKATWA ,WASIMAMA TENA GEITA

Mti huo, unaomilikiwa na Kanisa la Golan Gospel Center lililopo mtaani hapo, umeibua mijadala kuhusu uwezekano wa tukio hilo kuwa la miujiza.
Baadhi ya viongozi wa kanisa na wananchi wameeleza kushangazwa na hali hiyo.
Katibu wa Kanisa la GGC, Yohana Mathias, amesema tukio hilo limewashangaza waumini wa kanisa na wakazi wa Mpomvu, huku wengine wakilihusisha na nguvu za kiimani.
Mkazi wa Mpomvu, Emmanuel Lameck, amesema hajawahi kushuhudia jambo kama hilo maishani mwake na kwamba bado linafikirisha.
Naye Stella Saimon, mkazi wa Mpomvu, amekiri kuwa tukio hilo limeleta mshtuko kwa wengi, huku wengine wakitafsiri kuwa ni tukio la kiimani au la kishirikina.
Mchungaji wa Kanisa la Golan Gospel Center, Jefta Lameck, amesema mti huo ulikuwa wa muda mrefu, na baada ya kuangushwa na upepo, waliamua kuukata kwa kuwa ulikuwa umezuia njia. Hata hivyo, walipofika asubuhi iliyofuata, walikuta mti huo umesimama tena hali iliyozua mshangao mkubwa.
Amesema tukio hilo lisihusishwe na imani za kishirikina na amewataka wananchi kuwa watulivu huku wakilitafakari kwa mtazamo wa kawaida wa kimaumbile badala ya kuingiza hofu au imani potofu.
Chanzo - Maduka Online Blog
Wamarekani Hawautaki Ushirikiano wa TRUMP na Elon Mask, Washambulia Magari ya Tesla
Mashambulizi dhidi ya vituo vya Tesla yameongezeka baada ya #ElonMusk kushirikiana na utawala wa #Trump kwenye Idara ya Ufanisi wa Serikali (#DOGE), ambayo imepunguza matumizi makubwa ya serikali.
Miji kama Portland na Seattle imeathirika zaidi, huku magari ya Tesla, vituo vya kuchaji, na stoo za magari vikilengwa. Kwenye shambulio moja #LasVegas, magari kadhaa yaliwashwa moto na neno "#resist" likaandikwa kwenye jengo.
Mwanasheria Mkuu wa Marekani, Pam Bondi, alisema watu watatu waliokamatwa kwa mashambulizi hayo wanakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 20 kwa ugaidi wa ndani.
Trump alitumia #TruthSocial kutangaza kuwa wahusika wanapaswa kufungwa kwa miaka 20 na kupendekeza wafungwe katika magereza ya #ElSalvador, akiyataja mashambulizi hayo kama ugaidi wa ndani. Alisisitiza kuwa Tesla ni "kampuni kubwa ya Marekani" na hata kununua gari lake la #Tesla kuonyesha uungaji mkono.
Friday, March 21, 2025
DR. MPANGO AWAFARIJI WAFIWA MSIBA WA HAWASSI
Ripoti Ya Ufuatiliaji wa Uwajibikaji wa Jamii Katika Malezi na Makuzi ya Awali ya Mtoto Yaonesha Changamoto Kadhaa Babati
Na John Walter -Babati
Marafiki wa Elimu wilaya ya Babati wamewasilisha ripoti ya ufuatiliaji wa uwajibikaji wa jamii katika malezi na makuzi ya awali ya mtoto.
Ripoti hiyo, iliyowasilishwa na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Mji wa Babati, Benjamin Richard, inaonesha changamoto mbalimbali zinazowakabili watoto katika malezi, usalama, na mazingira ya kujifunzia.
Utafiti huu ulifanyika katika kata nne za Babati ,Bagara, Maisaka na Nangara kwenye shule za Msingi 16, ambapo wadau mbalimbali walihojiwa, wakiwemo watendaji wa kata, wamiliki wa vituo vya kulelea watoto (day care), walimu, wawakilishi wa asasi za kiraia, viongozi wa serikali za mitaa na vijiji, pamoja na wazazi wenye watoto katika shule za awali.
Matokeo Muhimu ya Ripoti
Usalama wa Watoto Shuleni
- Kati ya shule 16 zilizotembelewa, hakuna hata moja yenye uzio, hali inayohatarisha usalama wa watoto.
- Shule nyingi zipo karibu na barabara, hivyo kuongeza hatari kwa watoto.
Adhabu kwa Watoto
- Asilimia 11.2 ya waliohojiwa walithibitisha kuwepo kwa adhabu za kuumiza katika baadhi ya shule.
- Hata hivyo, asilimia 60 ya wazazi na walimu walikiri kuwa shule ni salama na wanatambua umuhimu wa ulinzi na usalama wa watoto.
Afya na Mazingira ya Shule
- Asilimia 68 ya vyoo vya shule si salama kwa watoto, hali inayohatarisha afya zao.
- Ni shule tano pekee ndizo zenye vyoo maalum kwa wanafunzi wa awali.
Malezi na Muda wa Wazazi na Watoto
- Asilimia 93.7 ya watu 168 waliohojiwa walikiri kuwa wazazi wengi hawana muda wa kukaa au kucheza na watoto wao.
- Wazazi wengi wamekuwa wakiacha majukumu yao kwa wafanyakazi wa ndani, ambao mara nyingi huonekana kama mama na baba wa watoto hao.
Hatua Zinazochukuliwa
Baada ya uwasilishaji wa ripoti hii, Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha Marafiki wa Elimu Babati, Gaudencia Igoshalimo, amesema kuwa watarejea kwa wananchi kwa ajili ya kuhamasisha marekebisho ya changamoto zilizobainika.
Marafiki wa Elimu Babati, chini ya mwavuli wa HakiElimu, wanatekeleza miradi mbalimbali ya kuboresha mazingira ya watoto, ikiwa ni pamoja na:
- Ujenzi wa vyoo katika shule tano ili kuboresha usafi na usalama wa wanafunzi.
- Ujenzi wa bweni katika Shule ya Sekondari Nakwa, ambapo wazazi watachangia ujenzi wa msingi na HakiElimu itakamilisha mradi huo.
Wito kwa Wazazi
Wazazi wametakiwa kutenga muda wa kukaa na watoto wao badala ya kuwaachia malezi kwa wafanyakazi wa ndani pekee.
"Wazazi waache tabia ya kuwa bize na maisha huku wakitelekeza watoto wao, ni jukumu la mzazi kuhakikisha mtoto anapata malezi bora na muda wa kufundwa katika misingi sahihi ya maisha," ilisisitizwa katika ripoti hiyo.
Kwa hatua hii, Marafiki wa Elimu Babati wanaendelea kushirikiana na jamii kuhakikisha kuwa watoto wanalelewa katika mazingira salama, yenye afya, na yanayochochea maendeleo yao ya elimu na maisha kwa ujumla.
Picha mbalimbali wakati wa Uwasilishaji ripoti.
Bosi Hakujua Kama Nimemfunga Mke wangu
Jina langu Abdallah, unajua wahenga hawakukosea waliposema ukistaajabu ya musa utayaoana ya firauni, huu ni msemo ambao hadi sasa unaishi katika maisha ya watu na jamii kwa ujumla kutokana na matukio na visa mbalimbali vinavyowakumba.
Singependa kutaja jina langu kutokana sababu za kiusalama ila naishi nchini Kenya, nimeamua kuandika ujumbe huu baada ya Bosi wangu kuleta mambo ya ajabu sana, nayo ni kung'ang'ania kuzaa mtoto na mke wangu wa ndoa.
Hata hivyo, mke wangu hakujua kama nimemfunga, wala Bosi wangu hakujua hilo, hivyo nilipokuwa napata safari za kikazi nilikuwa na amani tele na furaha zaidi hasa kutokana na kuongezeka kwa fedha ambayo nilikuwa napatiwa kama posho ya kujikimu na safari.
Baada ya muda wa miezi kadhaa mke wangu aliniita chumbani na kuniambia Bosi wangu alikuwa akimtongoza na kumwambia anataka kuzaa naye kutokana anaona watoto wetu ni wazuri sana na wanavutia.
Mke wangu aliniambia kwa muda mrefu alifanya jambo hilo kuwa siri lakini anaona kadiri anavyofanya siri moyo wake unakosa amani kabisa kutokana na jinsi anavyosumbuliwa.
Alilia sana na kuniomba msamaha kwa kutunza siri hiyo ya ajabu ambayo ingeweza kumfanya akazaa nje ya ndoa yetu ambayo imedumu kwa miaka mingi sasa, huku ikiwa na amani na upendo.
Hadi kufika hapo nikajua kabisa dawa ya Kiwanga Doctors kweli inafanya kazi yake ipasavyo, kilichokuja kunishangaza ni yule Bosi wangu alikuja kufukuzwa kazi katika mazingira ambayo sikuwahi kuyaelewa hadi sasa na hapo ndoa yangu ikazidi kuwa na usalama zaidi.
Unajua tulifikaje hapo?. kwa uwezo wa Kiwanga Doctors kutoka Migori, Kenya ndipo nilipobaini mbinu hiyo chafu ya Bosi wangu, nakumbuka nafiki yangu mmoja alinipa namba ya mtaalamu huyo na kuniambia anaweza kumfunga mke wangu asiweze kutoka nje ya ndoa.
Nilifika ofisini kwake na alinipatia dawa na kuanza kuzitumia, niliendelea na shughuli zangu, wakati huo Bosi wangu alikuwa kila mara ananipa safari nyingi za kikazi ili apate muda wa kuendelea kumshawishi mke wangu bila kujua tayari nilishamfunga.
Kwa hakika ni watu wengi wamepata uponyaji, mafanikio, furaha kupitia huduma za Kiwanga Doctors ambao unaweza kuwasiliana na kwa namba +254 116469840 au tembelea tovuti yao, www.kiwangadoctors.co.tz kwa maelezo zaidi kuhusu huduma zao.
Ommy Dimpoz Amefukuzwa na GSM na kuachishwa Kazi? Aandika haya baada ya tetesi kusambaa
Ommy Dimpoz amefukuzwa na GSM na kuachishwa kazi? Aandika haya baada ya tetesi kusambaa
Thursday, March 20, 2025
JUHIBU Yaja na Mbinu Mpya Kukabiliana na Wanyamapori Waharibifu
Na John Walter -Babati
Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Burunge (JUHIBU) imeendelea kubuni mbinu mbalimbali za kuzuia wanyamapori waharibifu kuvamia mashamba na kula mazao ya wakulima.
Katika juhudi hizo, JUHIBU imeanzisha matumizi ya baruti, pilipili na mchanga vilivyowekwa kwenye mipira ya kondomu kama moja ya njia za kuwazuia wanyama hao kuingia kwenye mashamba ya wananchi.
Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Kaganda, amekabidhi vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni 76 vya kuimarisha ulinzi wa mashamba kwa vijiji 10 vya kata ya Mwada, Nkaiti na Magara vinavyohudumiwa na JUHIBU.
Kwa mujibu wa Katibu wa JUHIBU Benson Mwaise, Vifaa hivyo ni pamoja na vilipuzi na honi, ambavyo vinalenga kusaidia wakulima kuwatisha wanyama waharibifu na hivyo kuwaepusha na hasara ya mazao yao.
Amesema kuwa hatua hiyo inalenga kupunguza migogoro kati ya binadamu na wanyamapori, hasa katika maeneo yanayopakana na hifadhi za wanyama.
"Tunapenda kuona wakulima wakiendelea kufanya shughuli zao bila hofu ya wanyama waharibifu, huku tukihakikisha kuwa wanyama hawa wanahifadhiwa kwa njia endelevu," alisema Kaganda.
JUHIBU imekuwa mstari wa mbele katika kutafuta suluhisho endelevu kwa changamoto hiyo, kwa kushirikiana na serikali na wananchi kuhakikisha wanyama na binadamu wanaishi kwa amani bila kuathiri ustawi wa pande zote mbili.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...