Saturday, April 5, 2025

RAIS SAMIA AZINDUA JENGO LA MAKAO MAKUU YA MAHAKAMA TANZANIA DODOMA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Aprili 5, 2025, amezindua rasmi Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania, pamoja na Jengo la Utumishi wa Mahakama na Makazi ya Majaji katika eneo la Tambukareli, Jijini Dodoma. 

Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Mahakama na wadau wa sekta ya sheria nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Samia amepongeza jitihada za Mahakama ya Tanzania katika kuboresha mazingira ya utoaji haki kwa kujenga miundombinu ya kisasa itakayowezesha watumishi wa mahakama kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi. 

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuiunga mkono Mahakama kwa kuimarisha mifumo ya kisasa ya teknolojia ya habari na mawasiliano katika shughuli zake.

Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, naye alikuwepo kushuhudia tukio hilo muhimu.

 Ameeleza kuwa uzinduzi wa majengo hayo ni hatua kubwa katika maboresho ya mfumo wa utoaji haki na ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya awamu ya sita ya kuimarisha taasisi za sheria nchini. 

Ameongeza kuwa majengo hayo yatasaidia kuongeza ufanisi na uwajibikaji kwa watumishi wa mahakama.

Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania pamoja na miundombinu mingine iliyozinduliwa leo linaonyesha dhamira ya dhati ya Serikali ya kuimarisha utawala wa sheria na kuwapatia wananchi huduma bora za kimahakama. 

Aidha, Makazi ya Majaji yaliyoko katika eneo hilo yanalenga kuboresha ustawi na mazingira ya kazi kwa majaji nchini.

Hafla hiyo imefanyika kwa shamrashamra huku wananchi wa Dodoma wakijitokeza kushuhudia tukio hilo la kihistoria. 

Uwepo wa Rais Samia Suluhu Hassan kama mgeni rasmi umeongeza uzito wa hafla hiyo, ikiwa ni ishara ya kuendelea kuimarisha mhimili wa Mahakama kama nguzo muhimu ya utawala bora nchini.
   

Friday, April 4, 2025

Ahmed Ally, Adui wa Yanga ni Rafiki Yetu, Tunamwalika RC Chacha Kwa Mkapa




"Tunafanya utaratibu wa kumwalika Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha aje kujumuika na Watanzania wenzake kuangalia mwakilishi wa nchi akienda nusu fainali. Tunamwalika sababu ya mchango wake wa kuhamasiha michezo na ajifunze namna maandalizi ya kimataifa yanafanyika kwa ajili ya kuiandaa timu yake ya Tabora United."- Semaji Ahmed Ally kwenye uzinduzi wa Kispika

TAFITI ZA KISAYANSI ZINACHOCHEA MABORESHO YA HUDUMA ZA AFYA NCHINI




Na Dotto Kwilasa,Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Afya imesema imeendelea kushirikiana na taasisi za utafiti, wadau wa maendeleo na sekta binafsi ili kuhakikisha tafiti zinazofanyika nchini zinagusa mahitaji halisi ya wananchi na kuchangia utekelezaji wa mipango ya maendeleo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe ameeleza kauli hiyo jijini Dodoma, Aprili 4, 2025 wakati wa Ufunguzi wa Mdahalo wa Kitaaluma (Symposium) katika Maadhimisho ya Wiki ya Afya Kitaifa.

amesema kuwa tafiti katika sekta ya afya ni nyenzo muhimu katika kuhakikisha huduma bora na zenye tija kwa wananchi, hasa kupitia tafiti za magonjwa ya binadamu ambazo ni sehemu ya mkakati wa kitaifa wa kuboresha afya ya jamii.

"Tafiti mbalimbali, hasa katika maeneo ya magonjwa kama vile Malaria, Kifua kikuu na yale ya kuambukiza, zimekuwa chachu ya mabadiliko chanya kwenye sera na mbinu za utoaji huduma," amesema Dkt. Shekalaghe.


"Tafiti zimetuwezesha kuwa na ushahidi wa kisayansi unaoongoza matumizi ya dawa mpya, mbinu bora za kinga na pia kubaini maeneo yenye changamoto kubwa zaidi kiafya," amesema Dkt. Shekalaghe.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe amesema mdahalo huo wa kitaaluma utasaidia katika kusukuma mbele maendeleo ya sekta ya afya nchini.

Naye, Mkurugenzi wa Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Dkt. Rashid Mfaume amesema kuwa hakuna halmashauri nchini isiyokuwa na hospitali, jambo linalothibitisha mafanikio ya uwekezaji mkubwa wa Serikali katika sekta ya afya.

Maadhimisho ya Wiki ya Afya kitaifa yenye Kauli mbiu isemayo " Tulipotoka, Tulipo, Tunapoelekea; Tunajenga Taifa Imara Lenye Afya" yanafayika kuanzia Machi 3 hadi 8 Aprili, 2025 katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete, jijini Dodoma, yakihusisha utoaji wa huduma za afya bure, maonesho ya taasisi, vipimo, chanjo pamoja na mijadala ya kitaalam.

JAMBO GROUP WARNS AGAINST JOB FRAUD

Jambo Group of Companies has issued a public warning regarding an increase in fraudulent activities involving individuals falsely representing themselves as company representatives. According to the company's statement, these fraudsters are contacting people both within and outside Tanzania, using fake documents to promise employment or high-paying contracts in exchange for fees.

The company has emphasized that it does not charge any fees for recruitment or contracting. All job application processes, including interviews and hiring, are completely free. Any request for payment should be considered fraudulent and reported immediately.

According to the statement, legitimate job and contract opportunities are only advertised through the company's official website (www.jambogroup.co.tz) and Instagram page (@jambogroup). Any communication from other sources should be treated with suspicion and verified using official contact details.

The public is urged to exercise caution and avoid making any payments if requested. Those who encounter such fraudulent attempts are advised to report the incident to local law enforcement or contact Jambo Group directly at info@jambogrouptz.net or +255 622 666 692.

Jambo Group of Companies has strongly condemned these fraudulent activities and reaffirmed its commitment to protecting the public from such scams. The company encourages everyone to remain vigilant and rely solely on official communication channels for accurate information.


Aziz K Ashikilia Namba 4 Kwa Wachezaji Wazawa wa Ndani Afrika wanaolipwa Mkwanja Mrefu




Kupitia kwenye Jarida la Africa Facts Zone limetoa orodha ya Wachezaji wanaolipwa mkunjwa mrefu zaidi kwa mwaka kwa wachezaji wanaochezea soka la ndani ya Afrika.

Katika Orodha hiyo Mchezaji anayeongoza ni Raia wa Misri anayechezea klabu ya Al ahly Ali Maaloul ambaye ni beki wa Kushotoa akilipwa dola milioni 1.5 ambayo ni zaidi ya Tsh bilioni 3 kwa Mwaka.

Aziz Ki kutoka klabu ya Yanga yupo nafasi ya Nne akilipwa dola laki mbili na elfu Arobani ambayo ni zaidi ya milioni 640 kwa Mwaka akiwa Yanga.

Mshahara huo kwa mwaka maana yake kwa mwezi analipwa dole Elfu Ishirini ambayo ni sawa milioni 53 za Kitanzania kwa mmoja.

Kwa maana hiyo Aziz Ki ndio mchezaji anayeongoza kulipwa mkwanja Mrefu zaidi Afrika Mashariki na Kati.

Mukwala wa Simba nafasi ya 6 akilipwa dola $108,000 ambayo ni zaidi ya milioni 288 za Kitanzania na kwa Mwezi analipwa dola 9,000 zaidi ya Tsh milioni 24 kwa Mwezi Simba.

Orodha hiyo hii hapa chini.

Highest Paid Players in African Leagues Annually -

1. Egypt - Ali Maaloul | $1.5 million | Al Ahly

2. South Africa - Ronwen Williams >= | $320,000 | Mamelodi Sundowns

3. Angola - Tiago Azulão | $263,000 | Petro de Luanda

4. Tanzania - Young Africans SC - Stephane Aziz Ki & $240,000 |

5. Rwanda- APR FC - Richmond Lamptey & | $120,000 /

6. Tanzania Mukwa Simba $108,000

7. . Zimbabwe- Scotland FC - Khama Billiat 1$72,0001

8. Nigeria- Stars • - Sikiru Alimi L | $10,163 | Remo

9. Eswatini - Neliswa Dlamini Nsingizini Hotspurs FC

Kwa Orodha hii unahisi mchezaji gani anashika nafasi ya tatu kutoka Tanzania baada ya Aziz Ki??

Swipe kuiona Orodha Yote.

Imeandikwa na @el_mando_tz

MBINU SHIRIKISHI NI MUHIMU KUHAKIKISHA WATU WENYE ULEMAVU WANAJUMUISHWA KATIKA NYANJA ZOTE– MHE. NDERIANANGA



NA. MWANDISHI WETU BERLIN – UJERUMANI

Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, na Uratibu, Mheshimiwa Ummy Nderiananga amesema ni muhimu kuwa na mbinu shirikishi ili kuhakikisha watu wenye ulemavu wanajumuishwa kikamilifu katika juhudi za maendeleo kitaifa na kimataifa.

Mhe. Ummy amesema hayo aliposhiriki katika mjadala wa: Kuelekea Hatua Jumuishi za Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi Kutoka Berlin hadi Belèm na Zaidi : wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Watu Wenye Ulemavu uliofanyika Berlin Ujerumani tarehe 2-3 Aprili, 2025.

Amesema kuwa ingawa serikali, wadau, na mashirika ya kimataifa wanafanya kazi ya kujenga jamii jumuishi, bado watu wenye ulemavu wanakabiliwa na changamoto nyingi.

"Changamoto hizi zinahitaji suluhisho la pamoja na la muda mrefu ili kuhakikisha fursa sawa na upatikanaji wa rasilimali kwa wote, bila kumwacha mtu yeyote nyuma," alisisitiza Mhe. Ummy.

Akizungumzia mifano ya mafanikio katika sera za ujumuishi wa watu wenye ulemavu kwenye masuala ya tabianchi, Mhe. Nderiananga alisema kuwa Serikali ya Tanzania imeweka sera, sheria, na mikakati mbalimbali kuhakikisha ujumuishi wa watu wenye ulemavu, hususan katika masuala ya menejimenti ya maafa na mabadiliko ya tabianchi.

Alitaja juhudi muhimu zilizofanywa na serikali kuwa ni pamoja na: Mifumo ya Usimamizi wa Maafa, ili kuhakikisha uwakilishi wa watu wenye ulemavu na kuzingatia mahitaji yao katika kukabiliana na majanga na urejeshaji wa hali baada ya maafa; Sera za Mabadiliko ya Tabianchi, zinazolenga kuimarisha ustahimilivu wa watu wenye ulemavu kwa hatua za kukabiliana na athari za tabianchi;

Mikakati Jumuishi ya Kukabiliana na Maafa, ikizingatia njia salama za uokoaji na mipango ya kuwahamisha watu wenye ulemavu; na Misaada ya Kijamii na Kisaikolojia, ili kusaidia watu wenye ulemavu wakati wa majanga

Aliziambia nchi nyingine kuwa zinaweza kujifunza kutoka Tanzania kwa kushirikiana na mashirika ya watu wenye ulemavu, kuunda sera jumuishi, kuhakikisha miundombinu inafikika, kufanya tathmini za athari, na kutenga fedha maalum kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

"Hatua hizi zinahakikisha kuwa watu wenye ulemavu hawataachwa nyuma katika maandalizi ya kukabiliana na majanga na ustahimilivu wa tabianchi," alisema, huku akialika mataifa mengine kuja Tanzania kujifunza juhudi zinazofanywa na serikali.

Kuhusu hatua mahsusi za ujumuishaji wa watu wenye ulemavu katika COP30 na sera za tabianchi, Mhe. Nderiananga alisema kuwa Tanzania imeweka mfumo madhubuti wa ujumuishaji watu wenye ulemavu katika mabadiliko ya tabianchi na usimamizi wa maafa kupitia sera, sheria, na miongozo mbalimbali.

Alisisitiza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na COP na wadau wengine ili kuhakikisha ujumuishaji kamili wa watu wenye ulemavu katika hatua za kukabiliana na tabianchi na itaendelea kushirikiana na mataifa mengine na mashirika ya kimataifa kuhimiza ajenda ya ujumuishaji wa watu wenye ulemavu katika COP30.




Sababu 7 Kwanini Waafrika Wanampenda Sana Ibrahim Traoré



 Sababu 7 Kwanini Waafrika Wanampenda Sana Ibrahim Traoré


MHE.NDERIANANGA AKUTANA NA MAKAMU WA RAIS IFAD


Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, na Uratibu, Mhe. Ummy Nderiananga, amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bi. Gérardine Mukeshimana, katika kikao cha pembezoni mwa Mkutano wa Kimataifa wa Watu Wenye Ulemavu uliofanyika tarehe 2–3 Aprili 2025 mjini Berlin, Ujerumani.

Katika mazungumzo hayo, Mhe. Ummy amesisitiza dhamira ya Serikali ya Tanzania kuendeleza ushirikiano na IFAD katika kuimarisha miradi ya kilimo inayolenga kuwawezesha watu wenye ulemavu, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa maendeleo jumuishi.

Viongozi hao wamejadili umuhimu wa kuweka mikakati madhubuti ya maendeleo jumuishi ili kuhakikisha programu za kilimo zinakuwa shirikishi, zenye usawa, na zenye manufaa kwa jamii nzima.

Kupitia IFAD, Tanzania inaendelea kutekeleza Mradi wa Maendeleo ya Kilimo na Uvuvi (AFDP) na Mradi wa Mageuzi ya Sekta ya Maziwa kwa Njia Endelevu ya Hali ya Hewa (C-SDTP), miradi inayochangia ustawi wa wananchi na kujenga mazingira jumuishi kwa watu wenye ulemavu katika sekta ya kilimo na mifugo.

Thursday, April 3, 2025

JENGO LA SITA KWA UKUBWA AFRIKA KUZINDULIWA DODOMA,NI MAKAO MAKUU YA MAHAKAMA YA TANZANIA




Na Dotto Kwilasa, Dodoma

Jumla ya Shilingi bilioni 129.7 zimetumika kugharamia ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania, ambalo linatajwa kuwa ni moja ya miradi mikubwa zaidi ya kimkakati kuwahi kutokea nchini. Jengo hili pia linatarajiwa kuwa kubwa zaidi barani Afrika na kushika nafasi ya sita kwa ukubwa duniani.

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel, alieleza hayo leo, Aprili 3, 2025, katika mkutano wake na vyombo vya habari, ambapo alisisitiza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, atazindua rasmi jengo hilo Aprili 5, mwaka huu.

Jengo hilo linajumuisha sehemu tatu kuu: Mahakama ya Upeo (Supreme Court), Mahakama ya Rufani, na Mahakama Kuu. Ujenzi wake umefadhiliwa kwa fedha za ndani, ikiwemo kodi za wananchi, na linatarajiwa kuwa na ukubwa wa mita za mraba 63,244. Aidha, jengo hili limejengwa kwa kuzingatia ubora wa kipekee na lengo la kudumu kwa zaidi ya miaka 100.

Prof. Gabriel amefafanua kuwa jengo hili litakuwa na mifumo ya kisasa ya TEHAMA, akili bandia, na roboti zitakazosaidia wananchi katika kutafuta ofisi mbalimbali, pamoja na sehemu ya kutua helikopta. Jengo hili linatarajiwa kuwa kitovu cha utoaji haki nchini, na limejengwa kwa lengo la kuboresha huduma za mahakama na kuongeza ufanisi wa kazi za utawala.

Mbali na uzinduzi wa jengo la Makao Makuu ya Mahakama, Rais Samia pia atazindua miradi mingine miwili, ikiwemo jengo la Makao Makuu ya Tume ya Utumishi wa Mahakama lenye ghorofa sita, lililogharimu Shilingi bilioni 14.3, pamoja na makazi ya majaji yenye thamani ya Shilingi bilioni 42.3.

Hafla hiyo ya kihistoria inatarajiwa kuhudhuriwa na zaidi ya wageni 2,500, wakiwemo viongozi kutoka sekta mbalimbali za serikali, bunge, mahakama, mashirika ya kiraia, na viongozi wa dini.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...