Saturday, July 17, 2021

VIDEO: Mwanamke akamatwa kwa kumchoma moto mpenzi wake ndani ya nyumba


Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia Grace Janes Mushi (25) kwa tuhuma za kumchoma moto ndani ya nyumba aliyekua mpenzi wake aliyefahamika kwa jina la Khamis Abdallah (25).

Tukio hilo limetokea  tarehe 16.07.2021 majira ya saa nane na nusu usiku huko maeneo ya Mbezi Makabe kwa Mzungu Wilaya ya Ubungo.

Mtuhumiwa Grace majira hayo ya saa nane usiku aliamka na kumfungia mlango kwa nje Khamis Abdallah kisha kumwagia mafuta ya petroli nyumba hiyo, kitendo kilichopelekea Khamisi kuungua na  kufariki dunia akiwa ndani. 

Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa kimapenzi.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.....USISAHAU KUSUBSCRIBE
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...