Friday, June 25, 2021
Bunge lapata wawakilishi 20 wa mabunge mengine Duniani
Wabunge Ishirini wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamechaguliwa kuliwakilisha bunge hilo katika mabunge mengine duniani, na wengine sita wamechaguliwa kuingia katika Tume ya Huduma za Bunge.
Wabunge hao wamechaguliwa baada ya majina yao kupitishwa kwenye Kamati za vyama vyao, lakini hawakupigiwa kura kutokana na idadi yao kulingana na nafasi zilizokuwa zikitakiwa.
Spika wa Bunge Job Ndugai ameliambia Bunge jijini Dodoma kuwa uchaguzi huo umefanyika kutokana na kuanza kwa bunge jipya la 12, baada ya waliokuwa Wawakilishi kumaliza muda wao.
Waliochaguliwa kwa kura ya ndio katika Bunge la dunia (APU) ni Esther Matiko, Mwanaisha Ulenge, Ramadhan Suleiman Ramadhan, Joseph Mhagama na Elibarick Kingu.
Kwa upande wa Bunge la Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) waliochaguliwa ni Shari Raymond, Kassim Hassan Haji, Seleman Zedi, Dkt. Afred Kimea na Hawa Mwaifunga.
Spika Ndugai amewataja Wabunge waliochaguliwa kuingia katika Bunge la Afrika kuwa ni Ngh'wasu Kamani, Turfik Salim Turik, Jerry Silaa, Nape Nnauye na Anatropia Theonest.
Waliochaguliwa kwenda Bunge la Umoja wa nchi za Maziwa Makuu ni Dkt. Christina Ishengoma, Najma Giga, Ezra Chiwelesa, Deus Sangu na Shamsia Mtamba.
Kwa mujibu wa taarifa ya Spika Ndugai Bungeni, Wabunge waliochaguliwa kuingia katika Tume ya Huduma za Bunge ni Aesh Hillary, Rashid Shangazi, Halima Mdee, Fakharia Shomari, Janejelly Ntate, Zahoro Mohamed na Khalifa Mohamed Issa.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
