Friday, June 25, 2021
Bunge lapata wawakilishi 20 wa mabunge mengine Duniani
Wabunge Ishirini wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamechaguliwa kuliwakilisha bunge hilo katika mabunge mengine duniani, na wengine sita wamechaguliwa kuingia katika Tume ya Huduma za Bunge.
Wabunge hao wamechaguliwa baada ya majina yao kupitishwa kwenye Kamati za vyama vyao, lakini hawakupigiwa kura kutokana na idadi yao kulingana na nafasi zilizokuwa zikitakiwa.
Spika wa Bunge Job Ndugai ameliambia Bunge jijini Dodoma kuwa uchaguzi huo umefanyika kutokana na kuanza kwa bunge jipya la 12, baada ya waliokuwa Wawakilishi kumaliza muda wao.
Waliochaguliwa kwa kura ya ndio katika Bunge la dunia (APU) ni Esther Matiko, Mwanaisha Ulenge, Ramadhan Suleiman Ramadhan, Joseph Mhagama na Elibarick Kingu.
Kwa upande wa Bunge la Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) waliochaguliwa ni Shari Raymond, Kassim Hassan Haji, Seleman Zedi, Dkt. Afred Kimea na Hawa Mwaifunga.
Spika Ndugai amewataja Wabunge waliochaguliwa kuingia katika Bunge la Afrika kuwa ni Ngh'wasu Kamani, Turfik Salim Turik, Jerry Silaa, Nape Nnauye na Anatropia Theonest.
Waliochaguliwa kwenda Bunge la Umoja wa nchi za Maziwa Makuu ni Dkt. Christina Ishengoma, Najma Giga, Ezra Chiwelesa, Deus Sangu na Shamsia Mtamba.
Kwa mujibu wa taarifa ya Spika Ndugai Bungeni, Wabunge waliochaguliwa kuingia katika Tume ya Huduma za Bunge ni Aesh Hillary, Rashid Shangazi, Halima Mdee, Fakharia Shomari, Janejelly Ntate, Zahoro Mohamed na Khalifa Mohamed Issa.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
