Wednesday, January 13, 2021
Fisi Azua Taharuki Shinyanga..... Ajeruhi Mzee Wa Miaka 70 Na Mwanae wa Miaka 17
SALVATORY NTANDU
Wakazi wawili wa Kijiji cha kilimawe kata ya Mwantini mkoani Shinyanga, Mabuga Ndakuna (70) na Timotheo Mabuga ( 17) wamejeruhiwa na mnyama aina ya fisi wakati wakijaribu kuokoa mifugo yao iliyokuwa kwenye banda la nyumba yao isishambuliwe na mnyama huyo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga (ACP) Debora Magiligimba amethibitisha kutokea kwa tukio hilo jana na kusema kuwa tukio hilo limetokea Januari 11 mwaka huu majira ya saa 10 alfajiri ambapo fisi huyo alivamia banda la kuku katika familia ya Mzee Mabuga na kushambulia kuku ndipo katika harakati za kumfukuza alianza kuwashambulia.
"Mzee Mabuga Ndakuna aling'atwa na kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo kichwani,miguuni na kuvunjwa mkono wa kushoto huku mwanae Timotheo aking'atwa sehemu mbalimbali za mwili wake kama vile mikono,miguuni na mabegani,"alisema Magiligimba.
Kamanda Magiligimba alisema kuwa chanzo cha tukio hilo ni mnyama huyo aina ya fisi kuvamia banda la kuku na wanafamilia hao kutoka nje kwenda kuokoa mifugo yao isiendelee kushambuliwa ambapo baada ya kutekeleza tukio hilo alikimbilia vichakani.
"Majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga, hali zao zinaendelea vizuri na jitihada za kumtafuta mnyama huyo zinaendelea ili kuwaondoa wanyama wakali katika kijiji hicho kwa kushirikiana na maafisa wanyama pori,"alisema Magiligimba.
Mwisho.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
